Swali: Ni ipi hekima baadhi ya Rak´ah katika kumi la mwisho la Ramadhaan ni ndefu katika kisomo chake, Rukuu´ zake na Sujuud zake na Rak´ah nyenginezo ni fupi?
Jibu: Kutokana na ninavyojua hakuna Sunnah Swahiyh inayojulisha juu ya hilo kwa upambanuzi. Lakini watu wamezowea hivo kwa ajili ya kuwakhafifishia watu na kuwapendezeshea kusimamisha swalah ya usiku. Atakayekhafifisha au akarefusha sehemu ya mwanzo ya usiku au mwishoni mwake hapana vibaya, pamoja na kuzingatia kuweka wazi kisomo, kuwa na unyenyekevu ndani yake na kuwa na utulivu ndani ya swalah na kutofanya haraka.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/20354/بيان-الحكمة-في-اطالة-صلاة-القيام-في-رمضان
- Imechapishwa: 19/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)