Swali: Mtu akifa hali ya kuwa yuko juu yake na siku za Ramadhaan au nadhiri familia yake wamfungie au wamtolee kafara badala ya kumfungia?
Jibu: Ikiwa alipona na akaweza kufunga lakini hata hivyo akafa kabla ya kufunga imesuniwa kwa ndugu zake kumfungia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayekufa na juu yake yuko na swawm basi walii wake amfungie.”[1]
Walii ni yule mtu wa karibu kama vile baba, mtoto, binadamu na wengineo.
Ikiwa maradhi yake yaliendelea mpaka akafa basi si yeye wala ndugu zake hawalazimiki kulipa wala kutoa fidia.
[1] al-Bukhaariy (02/240), Muslim (02/803), Ahmad (06/69) na wengineo.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/328-329)
- Imechapishwa: 18/06/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)