Swali: Vipi kuhusu kuomba du´aa ambazo hazikupokelewa katika Sujuud?
Jibu: Aombe kile anachotaka katika du´aa nzurinzuri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake anapokuwa amesujudu. Hivyo aombeni du´aa kwa wingi.”
Imekuja katika tamko jengine:
“Mja anakuwa karibu zaidi na Mola wake anapokuwa amesujudu. Hivyo basi, jitahidini katika du´aa.”
Swali: Bora si aombe du´aa zilizopokelewa?
Jibu: Sio lazima. Bora aombe yaliyopokelewa na ni sawa akiomba du´aa zingine. Watu wana mahitaji yao. Kwa hivyo ni sawa akiomba du´aa zilizopokelewa au akaomba du´aa nyenginezo.
Swali: Si jambo linalopingana na Sunnah?
Jibu: Haliendi kinyume na Sunnah. Aombe yale ambayo Allaah amemsahilishia.
Swali: Je, si imepokelewa kwamba achague katika du´aa zinazopendeza zaidi kwake?
Jibu: Hili ni kuhusu mwishoni mwa swalah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwafunza Maswahabah baada ya Tashahhud kwa kusema:
“Kisha achague katika du´aa inayopendeza zaidi kwake.”
Imekuja katika tamko jengine:
“Kisha achague katika mambo anayoyapenda mwishoni mwa swalah.”
Vivyo hivyo kuhusu du´aa katika Sujuud. Hukumu yake ni moja.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22790/هل-يجوز-الدعاء-في-السجود-بغير-الوارد
- Imechapishwa: 23/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)