Swali: Du´aa inayosema:
بسم الله اللهم جنبنا الشيطان وجنب الشيطان ما رزقتنا
“Naanza kwa jina la Allaah! Ee nilinde na shaytwaan na Kilinde na shaytwaan kile utachoturuzuku.”
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusiana na hili:
“Endapo Allaah amewaandikia kupata mtoto basi kamwe shaytwana hatomdhuru.”[1]
Aiseme mume baina yake yeye na nafsi yake?
Jibu: Ndio, mke asikie. Wote waseme:
بسم الله اللهم جنبنا الشيطان وجنب الشيطان ما رزقتنا
“Naanza kwa jina la Allaah! Ee nilinde na shaytwaan na Kilinde na shaytwaan kile utachoturuzuku.”
Mwanamke pia anatakiwa kusema hivo.
Swali: Je, aisome atapotaka kumwaga manii nje ya tupu ya mke?
Jibu: Aisome hata kama kumwaga manii nje ya tupu ya mke. Anaweza kutanguliwa na matamanio na asifikie lengo lake.
Swali: Lakini aisome kimyakimya?
Jibu: Aitamke.
[1] Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake (09/187) na waandishi wengine wa “as-Sunan” isipokuwa an-Nasaa´iy, katika “al-´Asharah” (01/79), ´Abdur-Razzaaq (06/193), at-Twabaraaniy (02/151/3) kupitia kwa Anas. Vilevile imepokelewa katika “al-Irwaa´-ul-Ghaliyl” (2012) kwa ukamilifu zaidi kuliko hapa.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23086/هل-الذكر-عند-الجماع-يقال-سرا
- Imechapishwa: 28/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)