Swali: Je, kusema ´Subhaan Allaah` baada ya Fajr mpaka kuchomoza kwa jua, kama ilivyokuja katika Aayah, ndio bora au kusoma Qur-aan? Ni upi wakati bora wa kuhifadhi Qur-aan?
Jibu: Bora ni kutilia umuhimu kusema ´Subhaan Allaah` na Adhkaar zilizowekwa katika Shari´ah. Lengo ni aifanye kila ´ibaadah ndani ya wakati wake mwishoni mwa mchana, mwanzoni mwa usiku au mwanzoni mwa asubuhi. Bora ni kutilia umuhimu Adhkaar na du´aa zilizowekwa katika Shari´ah. Ni sawa pia akisoma Qur-aan. Lakini akisoma Adhkaar zilizowekwa katika Shari´ah ni sawa kwa njia ya kwamba kila kitu akakiweka mahali pake. Kwa mfano katika Rukuu´ anatakiwa kusema:
سبحان ربي العظيم
“Ametakasika Mola wangu aliyetukuka.”
na asiombe du´aa. Aseme:
سبحان ربي العظيم
“Ametakasika Mola wangu aliyetukuka.”
Atapoinuka aseme:
سبحانك اللهم ربنا و وبحمدك,اللهم اغفر لي
“Kutakasika kutokamana na mapungufu ni Kwako ee Allaah, Mola wetu, na himdi zote unastahiki Wewe. Ee Allaah! Nisamehe!”
Baina ya Sujuud mbili aombe kwa kusema:
ربي اغفر لي، ربي اغفر لي
“Mola wangu nisamehe. Mola wangu nisamehe.”
Kila kitu akiweke mahali pake, ndio jambo lililowekwa katika Shari´ah. Akiomba du´aa kwa wingi, akasema ´Subhaan Allaah` kwa wingi, akasema ´Laa ilaaha illa Allaah` kwa wingi, akamtukuza Allaah na akakithirithisha du´aa zilizowekwa katika Shari´ah mida ya asubuhi na jioni ndio bora. Akisoma Qur-aan yote ni kheri tu.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23057/هل-التسبيح-بعد-الفجر-افضل-ام-التلاوة
- Imechapishwa: 30/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)