Kuhusu Sunnah, zipo dalili nyingi na nzuri zinazotilia nguvu kanuni iliyotangulia. Isitoshe hazikomeki na kitendo kimoja isipokuwa zinaenea katika vipengele vingine vilivyowekwa katika Shari´ah, kukiwemo usafi, swalah na mengine mengi. Ni ubainifu na upambanuzi wa yale yaliyotajwa kwa jumla katika Aayah za Qur-aan zilizotangulia juu ya suala hili. Hapa nakutajia nazo ili uwe juu ya ubainifu wa yale niliyoyasema…
Swalah:
1 – Abu ´Umar bin Anas amesimulia kutoka kwa mmoja katika ami zake wa ki-Answaar amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitafakari ni namna gani atawaita watu katika swalah ambapo akaambiwa: ”Simamisha bendera unapofika wakati wa swalah. Watu watakapoiona basi wataelezana.” Haikumpendeza. Ndipo kukatajwa pembe ya mayahudi. Haikumpendeza na akasema: ”Ni katika mambo ya mayahudi.” Ndipo kukatajwa kengele ya mnara ambapo akasema: ”Ni katika mambo ya manaswara.” ´Abdullaah bin Zayd bin ´Abdi Rabbih, ambaye aliguswa na jambo la Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), akaondoka na akaota adhaana usingizini mwake.”[1]
[1] Hadiyth ni Swahiyh na nimeitaja katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (511). Huko nimetaja wale maimamu walioisahihisha. Makusudio ya Hadiyth yako wazi kabisa.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Jilbaab-ul-Mar-ah al-Muslimah, uk. 167
- Imechapishwa: 30/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)