Swali: Kuna Hadiyth Swahiyh kuhusu kuangalia pale mahali mtu anaposujudu?
Jibu: Sikumbuki isipokuwa yale makatazo yanayokataza kunyanyua macho juu. Kumepokelewa matahadharisho ya kunyanyua macho juu.
Swali: Ni ipi Sunnah?
Jibu: Wajibu ni kuteremsha macho. Makatazo ya kunyanyua macho juu kunatoa faida kwamba ni lazima kuteremsha macho chini.
Swali: Vipi kuhusu kumtazama imamu?
Jibu: Sunnah ni pale mahali unaposujudia. Kwa sababu ndio jambo lililo karibu zaidi na unyenyekevu.
Swali: Kumepokelewa kitu kinacholengesha mahali pa kutazama wakati mtu anaswali kwa kuashiria na wakati wa Tashahhud?
Jibu: Sikumbuki kitu juu ya hayo. Muhimu ajitahidi ambacho kiko karibu zaidi na kumletea unyenyekevu.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22379/ما-دليل-النظر-الى-مكان-السجود-في-الصلاة
- Imechapishwa: 25/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)