Swali: Wako watenda madhambi wanasema kwamba hakuna dalili ya wazi kutoka ndani ya Qur-aan inayoharamisha sigara.
Jibu: Mwambie kuwa Allaah (Jalla wa ´Alaa) ameharamisha vibaya. Je, kitu hicho ni katika vitu vizuri au vibaya?
يَسْأَلُونَكَ مَاذَا أُحِلَّ لَهُمْ ۖ قُلْ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ
“Wanakuuliza wamehalalishiwa nini? Sema: “Mmehalalishiwa vilivyo vizuri.”[1]
Amesema alipokuwa akimsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
وَيُحِلُّ لَهُمُ الطَّيِّبَاتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيْهِمُ الْخَبَائِثَ
“Anawahalalishia vilivyo vizuri na anawaharamishia vichafu.”[2]
Isitoshe madaktari wamekubaliana na watu wakakubaliana kuwa madhara yake ni makubwa, kwamba inasababisha madhara mengi na shari nyingi. Kuna watu wengi wanaokufa kwa sababu ya sigara. Madhara haya yanatubainishia ubaya wake. Hata hivyo matamanio humfanya mtu akawa kipofu.
[1] 05:04
[2] 07:157
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21990/ما-الدليل-على-تحريم-الدخان
- Imechapishwa: 11/10/2022
Swali: Wako watenda madhambi wanasema kwamba hakuna dalili ya wazi kutoka ndani ya Qur-aan inayoharamisha sigara.
Jibu: Mwambie kuwa Allaah (Jalla wa ´Alaa) ameharamisha vibaya. Je, kitu hicho ni katika vitu vizuri au vibaya?
يَسْأَلُونَكَ مَاذَا أُحِلَّ لَهُمْ ۖ قُلْ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ
“Wanakuuliza wamehalalishiwa nini? Sema: “Mmehalalishiwa vilivyo vizuri.”[1]
Amesema alipokuwa akimsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
وَيُحِلُّ لَهُمُ الطَّيِّبَاتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيْهِمُ الْخَبَائِثَ
“Anawahalalishia vilivyo vizuri na anawaharamishia vichafu.”[2]
Isitoshe madaktari wamekubaliana na watu wakakubaliana kuwa madhara yake ni makubwa, kwamba inasababisha madhara mengi na shari nyingi. Kuna watu wengi wanaokufa kwa sababu ya sigara. Madhara haya yanatubainishia ubaya wake. Hata hivyo matamanio humfanya mtu akawa kipofu.
[1] 05:04
[2] 07:157
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21990/ما-الدليل-على-تحريم-الدخان
Imechapishwa: 11/10/2022
https://firqatunnajia.com/dalili-wapi-ndani-ya-qur-aan-kwamba-sigara-ni-haramu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)