Swali: Mtu anatamka shahaadah na akachinja kwa jila la Allaah lakini haswali. Je, ni halali kula kichinjwa chake?

Jibu: Ikiwa anaacha swalah kwa makusudi, si halali kichinjwa chake kwa sababu ameritadi kutoka katika Uislamu:

”Ahadi iliopo kati yetu sisi na wao ni swalah. Hivyo basi, yule atakayeiacha amekufuru.”[1]

[1] at-Tirmidhiy (2621), an-Nasaa’iy (463) na Ibn Maajah (1079). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (41)
  • Imechapishwa: 19/10/2023