as-Suhaymiy kuhusu mivutano ya ´Aliy al-Halabiy na al-Lajnah ad-Daaimah

Wenye haki ni al-Lajnah ad-Daa´imah. ´Aliy [bin] Hassan katika qadhiya hii alichanganya mambo. Alikosea kuipiga Radd al-Lajnah. Kwa kuwa hakuyafahamu maneno ya al-Lajnah, kamwe. Alikosea kupiga Radd al-Lajnah. Alikosea na kaidhulumu nafsi yake. Kafungua njia al-Lajnah kutukanwa bila ya kujua. Kafanya kosa, kafanya kosa, kafanya kosa, kafanya kosa mara elfu. Na yuko matamshi ambayo anawafungulia njia Murji-ah. Yuko na matamshi ambayo kunakhofiwa Murji-ah wakayatumia vibaya. Mfano wa hilo ni pale anaposema wakati fulani kuwa kuna kufuru ya matendo na I´tiqaad na kwamba mtu hakufuru isipokuwa akianguka tu katika kufuru ya I´tiqaad. Hili si sahihi. Hata Shaykh wake, Shaykh [Muhammad] Naaswir-ud-Diyn [al-Albaaniy] licha ya ubora wake na utukufu wake, hatukubaliani naye katika qadhiya hii. Kuna kufuru ya matendo ambayo inamtoa mtu katika dini. Kama kumtukana Allaah na Mtume Wake, kusujudia sanamu, kukejeli Sunnah. Yote haya ni kufuru inayomtoa mtu katika Uislamu.

  • Mhusika: Shaykh Swaalih bin Sa´d as-Suhaymiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=126980
  • Imechapishwa: 13/11/2022