Swali: Anayemuona mtu mwenye kuswali Sunnah wakati ambapo imamu anaswali faradhi.
Jibu: Afunzwe na abainishiwe. Haijuzu. Afunzwe kwamba kitendo hicho hakifai. Baadhi ya wanazuoni, kama wanazuoni wa Ahnaaf, wanaona kufaa kuswali Raatibah. Ni kosa. Ni maoni dhaifu.
Swali: Sunnah ya Fajr?
Jibu: Si Sunnah ya Fajr wala nyingine.
Swali: Lakini mtu anapata dhambi?
Jibu: Anayejua anapata dhambi. Na asiyejua pengine akapewa udhuru kutokana na ujinga wake. Lakini anapata dhambi baada ya kujua.
Swali: Swalah yake ya Sunnah inaharibika?
Jibu: Ndio, inaharibika.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22104/كيف-ينصح-من-يصلي-سنة-والامام-يصلي
- Imechapishwa: 27/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket