Swali: Ni zipi nasaha zako juu ya mtu ambaye anamtukana na kumtahadharisha Shaykh al-Albaaniy? Tunatakiwa tuchukue msimamo gani juu ya bwana huyu?
Jibu: Haya ni miongoni mwa maajabu makubwa kuona Shaykh al-Albaaniy anatahadharishwa, mtu ameitumikia Sunnah na kumaliza uhai wake katika kuzisoma Hadiyth za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuzihakiki na kubainisha ambazo ni Swahiyh na ambazo si Swahiyh. Kinyume chake inatakikana kwa mtu amwombee du´aa, amsifu na afaidike kutokana na elimu yake. Hii leo mtu ambaye anajishughulisha na Hadiyth hawezi kujitosheleza kurejea kwa watu wawili: Haafidhw Ibn Hajar na Shaykh al-Albaaniy. Faida inayoweza kuchumwa katika mambo yanayohusiana na Hadiyth kutoka kwa Ibn Hajar na Shaykh al-Albaaniy ni kubwa. Kwa ajili hiyo yule ambaye anamtahadharisha Shaykh al-Albaaniy basi anatahadharisha juu ya maarifa ya haki na Sunnah. Yale aliyofanya Shaykh al-Albaaniy juu ya Hadiyth ni huduma ya kipekee na uangalizi mtimilifu juu ya Sunnah na namna inavyotakiwa kutendewa kazi na kupokelewa na wanafunzi. Anastahiki kusifiwa na kuombewa du´aa.
- Mhusika: ´Allâmah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbâd
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=8mg9016GYTk
- Imechapishwa: 30/08/2020
Swali: Ni zipi nasaha zako juu ya mtu ambaye anamtukana na kumtahadharisha Shaykh al-Albaaniy? Tunatakiwa tuchukue msimamo gani juu ya bwana huyu?
Jibu: Haya ni miongoni mwa maajabu makubwa kuona Shaykh al-Albaaniy anatahadharishwa, mtu ameitumikia Sunnah na kumaliza uhai wake katika kuzisoma Hadiyth za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuzihakiki na kubainisha ambazo ni Swahiyh na ambazo si Swahiyh. Kinyume chake inatakikana kwa mtu amwombee du´aa, amsifu na afaidike kutokana na elimu yake. Hii leo mtu ambaye anajishughulisha na Hadiyth hawezi kujitosheleza kurejea kwa watu wawili: Haafidhw Ibn Hajar na Shaykh al-Albaaniy. Faida inayoweza kuchumwa katika mambo yanayohusiana na Hadiyth kutoka kwa Ibn Hajar na Shaykh al-Albaaniy ni kubwa. Kwa ajili hiyo yule ambaye anamtahadharisha Shaykh al-Albaaniy basi anatahadharisha juu ya maarifa ya haki na Sunnah. Yale aliyofanya Shaykh al-Albaaniy juu ya Hadiyth ni huduma ya kipekee na uangalizi mtimilifu juu ya Sunnah na namna inavyotakiwa kutendewa kazi na kupokelewa na wanafunzi. Anastahiki kusifiwa na kuombewa du´aa.
Mhusika: ´Allâmah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbâd
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=8mg9016GYTk
Imechapishwa: 30/08/2020
https://firqatunnajia.com/anamtahadharisha-al-albaaniy/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)