Swali: Je, eda ya mwanamke mjamzito inakwisha akijifungua punde tu baada ya mume wake kuaga dunia?
Jibu: Akijifungua kitambo kidogo tu baada kufariki mume wake, imemalizika eda yake:
وَأُولَاتُ الْأَحْمَالِ أَجَلُهُنَّ أَن يَضَعْنَ حَمْلَهُنَّ
”Na wenye mimba muda wao [wa eda] watakapozaa mimba zao.”[1]
Aayah hii ni kwa njia ya kuachia. Akijifungua kitambo kidogo tu baada ya yeye kuaga dunia, basi imemalizika eda yake. Baadhi ya wanazuoni, kama inavyonasibishwa kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa), wanaona kuwa anatakiwa kukaa ile eda ndefu zaidi katika eda mbili hizo, lakini haya sio maoni ya jopo la wanazuoni wengi, na isitoshe sio hayaafikiani na udhahiri wa inavosema Aayah.
[1] 65:04
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (40)
- Imechapishwa: 11/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)