Swali: Nilianza kufunga siku sita za Shawwaal lakini hata hivyo sikuweza kuikamilisha kutokana na baadhi ya mambo na kazi kwa vile nilibakiza siku mbili. Nifanye nini? Je, nizilipe? Je, napata dhambi kwa jambo hilo?
Jibu: Kufunga siku sita za Shawwaal ni ´ibaadah iliyopendekezwa na sio lazima. Kwa hivyo unapata thawabu kwa zile siku ulizofunga. Kunatarajiwa kwako kupata ujira kamili ikiwa kilichokuzuia kukamilisha ni udhuru unaokubalika katika Shari´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtu anapokuwa mgonjwa au akasafiri, basi Allaah anamwandikia mfano wa aliyokuwa akiyafanya katika hali ya ukazi na uzima.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake.
Hulazimiki kulipa yale uliyoacha.
[1] al-Bukhaariy (2996).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/395)
- Imechapishwa: 07/05/2022
Swali: Nilianza kufunga siku sita za Shawwaal lakini hata hivyo sikuweza kuikamilisha kutokana na baadhi ya mambo na kazi kwa vile nilibakiza siku mbili. Nifanye nini? Je, nizilipe? Je, napata dhambi kwa jambo hilo?
Jibu: Kufunga siku sita za Shawwaal ni ´ibaadah iliyopendekezwa na sio lazima. Kwa hivyo unapata thawabu kwa zile siku ulizofunga. Kunatarajiwa kwako kupata ujira kamili ikiwa kilichokuzuia kukamilisha ni udhuru unaokubalika katika Shari´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtu anapokuwa mgonjwa au akasafiri, basi Allaah anamwandikia mfano wa aliyokuwa akiyafanya katika hali ya ukazi na uzima.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake.
Hulazimiki kulipa yale uliyoacha.
[1] al-Bukhaariy (2996).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/395)
Imechapishwa: 07/05/2022
https://firqatunnajia.com/ameshindwa-kukamilisha-swawm-ya-shawwaal-kutokana-na-udhuru/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)