Swali: Nilisafiri katika Ramadhaan na nikala siku mbili ambazo nilinuia kuzifunga. Lakini sikuyakumbuka hayo isipokuwa baada ya kuingia Ramadhaan ya mwaka huu.
Jibu: Uhalisia ikiwa ni kama ulivosema basi huna dhambi kwa kuchelewesha siku mbili ulizokula mpaka kukaingia Ramadhaan nyingine. Unalazimika kuzilipa baada ya hapo. Imethibiti ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema ya kwamba Allaah (Subhaanah) amesema:
“Nimekwishafanya.”[1]
Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” yake:
“Atakayesahau na akala au kunywa basi atimize swawm yake. Kwani si vingine ni Allaah ndiye kamlisha na kumnywesha.”[2]
[1] 02:286
[2] al-Bukhaariy (1933), Muslim (1155), at-Tirmidhiy (721) na wengineo.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/336-337)
- Imechapishwa: 18/06/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket