al-Waadi´iy kwamba mke aliyejamiiwa mchana wa Ramadhaan hatoi kafara

Swali: Vipi ikiwa mwanamke alijaamiwa kwa ridhaa yake na hakumzuia mume wake kutokana na hilo?

Jibu: Anapata dhambi ikiwa naye ameridhia. Kusema kwamba na yeye atatoa kafara Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakumwamrisha kufanya hivo. Wala hakumwambia yule bwana amwamrishe mke wake ikiwa na yeye aliridhia kufanya hivo. Hata hivyo naye anapata dhambi ikiwa yeye ndiye amesababisha mpaka mume wake akaingia katika aliyoingia.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 81
  • Imechapishwa: 18/03/2024