Vipo vitabu vya wajinga wanaosema kuwa ad-Dajjaal hayupo. Wanasema kuwa hiyo ni ibara ya uongo mwingi katika zama za mwisho na kwamba hakuna jambo la kuteremka kwa ´Iysaa. Wanasema kuwa hiyo ni ibara ya kudhihiri kwa haki. Huku ni kupinga jambo lililopokelewa kwa wingi katika Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Bali Qur-aan imefahamisha juu ya kuteremka kwa ´Iysaa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Amesema (Ta´ala):
وَإِن مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ إِلَّا لَيُؤْمِنَنَّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ
“Hakuna yeyote katika Ahl-ul-Kitaab isipokuwa atamwamini kabla ya kufa kwake.”
Hii ni dalili juu ya kwamba atateremka katika zama za mwisho. Mayahudi waliomkufuru hapo mwanzo watamwamini:
وَإِن مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ إِلَّا لَيُؤْمِنَنَّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكُونُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا
“Hakuna yeyote katika Ahl-ul-Kitaab isipokuwa atamwamini kabla ya kufa kwake na siku ya Qiyaamah atakuwa shahidi juu yao.”[1]
Katika Aayah nyingine amesema juu ya ´Iysaa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
وَإِنَّهُ لَعِلْمٌ لِّلسَّاعَةِ
“Hakika yeye ni alama ya Saa.”[2]
Bi maana kuteremka kwake katika zama za mwisho ni alama za kukaribia kwa Qiyaamah. Kuna kisomo kinasomwa:
وَإِنَّهُ لَعِلَمٌ لِلسَّاعَةِ
“Hakika yeye ni alama ya Saa.“[3]
Kuteremka kwa ´Iysaa bin Maryam (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutoka mbinguni ni alama juu ya kukaribia kwa Qiyaamah. Ni miongoni mwa alama na ishara za Qiyaamah.
[1] 04:159
[2] 43:61
[3] Kimesomwa na Ibn ´Abbaas, Qataadah na adh-Dhwahhaak. Tazama ”Tafsiyr-ut-Twabariy” (25/90-91).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-il-Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 125-126
- Imechapishwa: 26/05/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)