Aliulizwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu njia ambapo akasema:
“Ni yenye kutelezesha na juu yake kuna makucha ya wanyama wakali, makucha kama ya mbwa na miba ilio sawa na mipana na ina miba inayoweza kuua mbuzi inakuweko Najd inaitwa “as-Sa´daan.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
Amepokea tena kutoka katika Hadiyth ya Abu Hurayrah:
“… ina makucha kama ya mbwa mfano wa makucha ya mti huyo wa as-Sa´daan licha ya kwamba hakuna anayejua ukubwa wake isipokuwa Allaah. Itawapora watu kutegemea matendo yao.”[2]
Katika “as-Swahiyh” ya Muslim kutoka katika Hadiyth ya Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesema:
“Nimefikiwa na khabari ya kwamba [hiyo Njia] ni nyembamba sana kuliko nywele na ina makali sana kuliko upanga.”[3]
Imaam Ahmad amepokea mfano wake kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Ni sehemu ya Hadiyth ya Abu Sa´iyd al-Khudriy iliyokwishatangulia aliyoipokea al-Bukhaariy na Muslim.
[2] al-Bukhaariy (6573) na Muslim (182, 299).
[3] Muslim (183, 302) iliyokwishatangulia.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 126-127
- Imechapishwa: 04/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)