Swali 73: Ni Aayah ipi ya mwisho iliyoteremka kutoka katika Qur-aan?
Jibu: Kwa mujibu wa al-Baraa´ bin ´Aazib ilikuwa:
يَسْتَفْتُونَكَ قُلِ اللَّـهُ يُفْتِيكُمْ فِي الْكَلَالَةِ
”Wanakuuliza hukumu ya Shari´ah. Sema: ”Allaah anakubainishieni kuhusu a asiye na watoto wala mzazi.”[1]
Kwa mujibu wa ´Umar Aayah ya mwisho kuteremshwa ilikuwa kuhusu ribaa.
Kwa mujibu wa Ibn Shihaab Aayah ya ribaa na Aayah ya deni ndio zilikuwa za mwisho kuteremka. Ibn ´Abbaas amesema:
”Cha mwisho kuteremshwa kutoka katika Qur-aan ilikuwa:
وَاتَّقُوا يَوْمًا تُرْجَعُونَ فِيهِ إِلَى اللَّـهِ ۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفْسٍ مَّا كَسَبَتْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ
”Iogopeni Siku mtakayorejeshwa kwa Allaah, kisha kila nafsi italipwa kamilifu iliyoyachuma, nao hawatodhulumiwa.”[2]
Hayohayo ndio yamesemwa na Abu Sa´iyd al-Khudriy. Ibn ´Abbaas amesema:
”Iliteremshwa siku kumi na tatu kabla ya kifo chake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”
Sa´iyd bin Jubayr amesema mfano wa hayo kuhusu Aayah ya mwisho na akaongeza:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliishi siku tisa baada ya kushushwa kwake. Kisha akafariki jumatatu wakati kumebakia siku mbili za Rabiy´ al-Awwal.”[3]
Huenda mwanzoni mwa Aayah ya ribaa hadi mwisho wa Aayah ya deni zilishushwa kwa pamoja – na Allaah ndiye mjuzi zaidi.
[1] 4:176
[2] 2:281
[3] Tafsiyr Ibn Abiy Haatim (2/554).
- Mhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 144
- Imechapishwa: 08/11/2023
Swali 73: Ni Aayah ipi ya mwisho iliyoteremka kutoka katika Qur-aan?
Jibu: Kwa mujibu wa al-Baraa´ bin ´Aazib ilikuwa:
يَسْتَفْتُونَكَ قُلِ اللَّـهُ يُفْتِيكُمْ فِي الْكَلَالَةِ
”Wanakuuliza hukumu ya Shari´ah. Sema: ”Allaah anakubainishieni kuhusu a asiye na watoto wala mzazi.”[1]
Kwa mujibu wa ´Umar Aayah ya mwisho kuteremshwa ilikuwa kuhusu ribaa.
Kwa mujibu wa Ibn Shihaab Aayah ya ribaa na Aayah ya deni ndio zilikuwa za mwisho kuteremka. Ibn ´Abbaas amesema:
”Cha mwisho kuteremshwa kutoka katika Qur-aan ilikuwa:
وَاتَّقُوا يَوْمًا تُرْجَعُونَ فِيهِ إِلَى اللَّـهِ ۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفْسٍ مَّا كَسَبَتْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ
”Iogopeni Siku mtakayorejeshwa kwa Allaah, kisha kila nafsi italipwa kamilifu iliyoyachuma, nao hawatodhulumiwa.”[2]
Hayohayo ndio yamesemwa na Abu Sa´iyd al-Khudriy. Ibn ´Abbaas amesema:
”Iliteremshwa siku kumi na tatu kabla ya kifo chake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”
Sa´iyd bin Jubayr amesema mfano wa hayo kuhusu Aayah ya mwisho na akaongeza:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliishi siku tisa baada ya kushushwa kwake. Kisha akafariki jumatatu wakati kumebakia siku mbili za Rabiy´ al-Awwal.”[3]
Huenda mwanzoni mwa Aayah ya ribaa hadi mwisho wa Aayah ya deni zilishushwa kwa pamoja – na Allaah ndiye mjuzi zaidi.
[1] 4:176
[2] 2:281
[3] Tafsiyr Ibn Abiy Haatim (2/554).
Mhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 144
Imechapishwa: 08/11/2023
https://firqatunnajia.com/73-ni-aayah-ipi-ya-mwisho-iliyoteremka-kutoka-katika-qur-aan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)