Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
55 – Kama ilivyotajwa na Kitabu cha Mola wetu:
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ
“Kuna nyuso siku hiyo zitanawiri. Zikimtazama Mola wake.”[1]
56 – Tafsiri yake ni kama alivokusudia Allaah (Ta´ala) na kujua.
MAELEZO
Aayah hii inasema wazi kwamba Allaah ataonekana kwa macho, kwa sababu kumetajwa kihusishi (إِلَى). Maana yake ni kuwa macho ndio yataona. Mu´tazilah wanasema kuwa (إِلَى) ni wingi wa neema. Kwa maana nyingine wataona neema za Mola wake. Makengeusho haya yanachekesha kwa sababu viambishi havina wingi. Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Tafsiri yake ni kama alivokusudia Allaah (Ta´ala) na kujua.”
Bi maana inatakiwa kufahamika kama alivyotaka Allaah, nako ni kuonekana kwa macho na si kama walivyofasiri wazushi.
[1] 75:22-23
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 79-80
- Imechapishwa: 17/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)