Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
… na Allaah akafaradhisha kwa viumbe wote – majini na watu – kumtii. Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا
“Sema: “Hakika mimi ni Mtume wa Allaah kwenu nyinyi nyote.””[1]
Allaah kupitia kwake ameikamilisha dini. Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا
”Leo nimekukamilishieni dini yenu na nimekutimizieni neema Yangu na nimekuridhieni kwenu Uislamu uwe ndio dini yenu.”[2]
Dalili ya kufa kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Kauli Yake (Ta´ala):
إِنَّكَ مَيِّتٌ وَإِنَّهُم مَّيِّتُونَ ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
“Hakika wewe utakufa na wao pia ni watakufa. Kisha hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenumtagombana.”[3]
MAELEZO
Kumtii Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni lazima kwa majini na watu wote. Yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Mtume wa Allaah kwenda kwa waarabu na wasiokuwa waarabu katika majini na watu. Majini wamefaradhishiwa mambo ya Shari´ah kama walivyofaradhishiwa watu. Dalili ni maneno Yake (Ta´ala):
وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِّنَ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنصِتُوا ۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَىٰ قَوْمِهِم مُّنذِرِينٍَ
”Wakati Tulipowaelekeza kwako kundi miongoni mwa majini wakisikiliza Qur-aan, walipoihudhuria walisema: “Nyamazeni [msikilize]!” Ilipokwisha [kusomwa], waligeuka kurudi kwa watu wao wakiwaonya.”[4]
وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَـٰذَا الْقُرْآنُ لِأُنذِرَكُم بِهِ وَمَن بَلَغَ
“Nimefunuliwa Wahy hii Qur-aan ili nikuonyeni kwayo na kila itakayomfikia.”[5]
تَبَارَكَ الَّذِي نَزَّلَ الْفُرْقَانَ عَلَى عَبْدِهِ لِيَكُونَ لِلْعَالَمِينَ نَذِيرًا
“Amebarikika Yule ambaye ameteremsha Pambanuzi kwa mja Wake ili awe ni muonyaji kwa walimwengu.”[6]
Mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) amesema:
“Dalili ya kufa kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)… “
Ameshakufa. Hata hivyo yuko hai uhai wa maisha ya ndani ya kaburi. Kiwiliwili chake kitukufu hakiliwi na ardhi. Bado ni kibichi na ni chenye kubaki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika Allaah (´Azza wa Jall) ameiharamishia ardhi kula miili ya Manabii.”[7]
Ama watu wengine miili yao haibaki na hakuna kinachobaki isipokuwa عجب الذنب ambacho ni kifupa kilicho kwenye uti wa mgongo wa mtu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kila mwana wa Aadam huliwa na udongo. Isipokuwa عجب الذنب; ameumbwa kwacho na hutengenezwa kwacho.”[8]
Mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) ametaja dalili ya kufa kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
إِنَّكَ مَيِّتٌ وَإِنَّهُم مَّيِّتُونَ
“Hakika wewe utakufa na wao pia ni watakufa.”
Baadhi ya watu huvutana ya kwamba hakufa. Vilevile dalili nyingine inayofahamisha juu ya kufa kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni maneno Yake (Ta´ala):
وَمَا مُحَمَّدٌ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ ۚ أَفَإِن مَّاتَ أَوْ قُتِلَ انقَلَبْتُمْ عَلَىٰ أَعْقَابِكُمْ ۚ
“Muhammad si chochote isipokuwa ni Mtume tu [na] wamekwishapita kabla yake Mitume [wengine]. Je, akifa au akiuawa mtageuka nyuma ya visigino vyenu?”[9]
[1] 07:158
[2] 05:03
[3] 39:30-31
[4] 46:29
[5] 06:19
[6] 25:01
[7] Abu Daawuud (1047), an-Nasaa´iy (1374) na Ibn Maajah (1085). al-Haakim amesema:
”Hadiyth hii ni Swahiyh juu ya sharti za al-Bukhaariy” lakini hakuipokea.
[8] Muslim (2955).
[9] 03:144
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 103-104
- Imechapishwa: 16/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)