Ndugu wapendwa! Hichi ni kikao cha pili katika kubainisha fungu la pili katika adabu za funga. Nazo ni zile adabu zilizopendekezwa. Miongoni mwazo ni:
Daku. Ni kule kula sehemu ya mwishoni ya usiku. Imepata jina hilo kwa sababu hutokea kipindi cha kabla ya kuingia alfajiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha daku pale aliposema:
“Kuleni daku. Kwani hakika katika kula daku kuna baraka.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Muslim amepokea vilevile katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kipambanuzi kati ya funga yetu na funga ya Ahl-ul-Kitaab ni kula daku.”
Amesifia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kula daku ya tende pale aliposema:
“Neema ya daku ya muumini ni daku.”
Ameipokea Abu Daawuud[1].
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Daku yote ni baraka. Msiiache ijapo ni kwa kuweka kinywani mwake maji. Kwani hakika Allaah na Malaika Wake wanawaswalia walaji daku.”
Ameipokea Ahmad. al-Mundhiriy amesema:
“Cheni ya wapokezi wake ni yenye nguvu.”[2]
Mlaji daku anatakiwa kunuia kwa daku lake kutekeleza amri ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumwigiliza kitendo chake ili daku hiyo iwe ni ´ibaadah na anuie kwa funga yake kumcha Allaah ili apate ujira.
[1] Cheni ya wapokezi wake ni nzuri. Ina shawahidi inayoifikisha katika daraja ya usahihi.
[2] Sentesi ya mwanzo ina shahidi kwa al-Bukhaariy na Muslim.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 75-76
- Imechapishwa: 24/04/2021
Ndugu wapendwa! Hichi ni kikao cha pili katika kubainisha fungu la pili katika adabu za funga. Nazo ni zile adabu zilizopendekezwa. Miongoni mwazo ni:
Daku. Ni kule kula sehemu ya mwishoni ya usiku. Imepata jina hilo kwa sababu hutokea kipindi cha kabla ya kuingia alfajiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha daku pale aliposema:
“Kuleni daku. Kwani hakika katika kula daku kuna baraka.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Muslim amepokea vilevile katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kipambanuzi kati ya funga yetu na funga ya Ahl-ul-Kitaab ni kula daku.”
Amesifia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kula daku ya tende pale aliposema:
“Neema ya daku ya muumini ni daku.”
Ameipokea Abu Daawuud[1].
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Daku yote ni baraka. Msiiache ijapo ni kwa kuweka kinywani mwake maji. Kwani hakika Allaah na Malaika Wake wanawaswalia walaji daku.”
Ameipokea Ahmad. al-Mundhiriy amesema:
“Cheni ya wapokezi wake ni yenye nguvu.”[2]
Mlaji daku anatakiwa kunuia kwa daku lake kutekeleza amri ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumwigiliza kitendo chake ili daku hiyo iwe ni ´ibaadah na anuie kwa funga yake kumcha Allaah ili apate ujira.
[1] Cheni ya wapokezi wake ni nzuri. Ina shawahidi inayoifikisha katika daraja ya usahihi.
[2] Sentesi ya mwanzo ina shahidi kwa al-Bukhaariy na Muslim.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 75-76
Imechapishwa: 24/04/2021
https://firqatunnajia.com/60-adabu-ya-kwanza-iliyopendekezwa-daku/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)