Swali 58: Baadhi ya watu wanawatukuza watu na kushabikia maoni yao. Unawanasihi nini watu hawa?
Jibu: Ni wajibu kufuata haki pamoja na yeyote yule atakayekuwa nayo[1], na si kuwafuata watu wanaopingana na haki. Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amesema:
”Nashangazwa na watu wanaoitambua haki ya wapokezi na usahihi wake lakini wanaiacha na kwenda katika maoni ya Sufyaan. Allaah (Ta´ala) amesema:
فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ
“Basi watahadhari wale wanaokwenda kinyume amri yake; isije kuwapata fitina au ikawapata adhabu iumizayo.”[2]
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
”Mawe yanakaribia kukushukieni kutoka mbinguni; nawaambie Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema na nyinyi mnasema Abu Bakr na ´Umar wamesema.”[3]
Ikiwa haya matahadharisho ni juu ya kuwafuata viumbe bora kabisa baada ya Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam) pasi na dalili, kusemwe nini juu ya kumfuata ambaye haitambuliki elimu wala ubora wake isipokuwa tu ni hodari wa kuongea?
[1] al-Awzaa´iy (Rahimahu Allaah) amesema:
”Tunazunguka na Sunnah kule inakoelekea.” (Sharh Usuwl I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah (1/64))
[2] 24:63
[3] Ahmad (3121).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ajwibah al-Mufiydah ´an As-ilat-il-Manaahij al-Jadiydah, uk. 158-159
- Imechapishwa: 24/03/2024
- Taaliki: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)