Swali 55: Imamu amewaswalisha maamuma pasi na wudhuu´ kwa kusahau. Ni ipi hukumu ya swalah hii katika hali zifuatazo:
1 – Akikumbuka jambo hilo katikati ya swalah?
2 – Akikumbuka baada ya salamu na kabla ya watu kuondoka?
3 – Akikumbuka baada ya watu kutawanyika?
Jibu: Akikumbuka baada ya kutoa salamu basi swalah ya maamuma ni sahihi na si lazima kwao kuirudia. Lakini imamu yeye atalazimika kuirudia.
Lakini akikumbuka katikati ya swalah basi anatakiwa kuteua ambaye atawakamilishia swalah yao kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni. Hilo ni kutokana na kisa cha ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) wakati alipodungwa ndani ya swalah alimteua ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf (Radhiya Allaahu ´anh) ambapo akawakamilishia swalah na hakuianza mwanzo.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 59-60
- Imechapishwa: 07/09/2022
Swali 55: Imamu amewaswalisha maamuma pasi na wudhuu´ kwa kusahau. Ni ipi hukumu ya swalah hii katika hali zifuatazo:
1 – Akikumbuka jambo hilo katikati ya swalah?
2 – Akikumbuka baada ya salamu na kabla ya watu kuondoka?
3 – Akikumbuka baada ya watu kutawanyika?
Jibu: Akikumbuka baada ya kutoa salamu basi swalah ya maamuma ni sahihi na si lazima kwao kuirudia. Lakini imamu yeye atalazimika kuirudia.
Lakini akikumbuka katikati ya swalah basi anatakiwa kuteua ambaye atawakamilishia swalah yao kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni. Hilo ni kutokana na kisa cha ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) wakati alipodungwa ndani ya swalah alimteua ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf (Radhiya Allaahu ´anh) ambapo akawakamilishia swalah na hakuianza mwanzo.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 59-60
Imechapishwa: 07/09/2022
https://firqatunnajia.com/55-imamu-amewaswalisha-maamuma-bila-wudhuu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)