Kuna aina mbili za upamoja wa Allaah (المعية) na viumbe Wake:
1 – Upamoja wenye kuenea kwa muumini na kafiri. Allaah yuko pamoja na waumini na makafiri kwa kuwaona, kuwachunga na kupitisha uwezo na matakwa Yake:
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ وَاللَّهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ
”Naye Yu Pamoja nanyi popote mlipo. Na Allaah kwa myatendayo ni Mwenye kuyaona.”[1]
2 – Upamoja maalum kwa waumini na Mitume. Amesema (Ta´ala):
إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الَّذِينَ اتَّقَوا وَّالَّذِينَ هُم مُّحْسِنُونَ
“Hakika Allaah Yu Pamoja na wenye kumcha na wale watendao wema.”[2]
Kwa hivyo Yeye yuko pamoja na wenye kumcha na pamoja na wafanyao wema kwa kuwanusuru, kuwatia nguvu, kuwawafikisha, kuwafanya imara na wakati huohuo yuko juu ya ´Arshi. Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu Muusa na Haaruun:
قَالَ لَا تَخَافَا ۖ إِنَّنِي مَعَكُمَا أَسْمَعُ وَأَرَىٰ
“Hakika Mimi Niko pamoja nanyi, Nasikia na Naona.”[3]
Amesema kuhusu Mtume wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati alipokuwa katika pango la Hiraa´ pamoja na Abu Bakr as-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh):
لاَ تَحْزَنْ إِنَّ اللّهَ مَعَنَا
“Usihuzunike – hakika Allaah Yu Pamoja nasi!”[4]
[1] 57:04
[2] 16:128
[3] 20:46
[4] 09:40
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 81
- Imechapishwa: 14/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)