Kuhusu wale Maswahabah ambao wameshuhudiwa na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa dhati zao ya kwamba ni katika watu wa Peponi, basi Ahl-ul-Hadiyth wanafanya vivyo hivyo juu yao kwa sababu ya kusadikisha maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na ahadi yake kwao. Kwani hakika yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hawakushuhudia hayo isipokuwa baada ya kuyatambua hayo. Allaah (Ta´ala) alifichulia Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yale Aliyoyataka katika yaliyofichikana. Dalili ya hilo ni katika maneno Yake (´Azza wa Jall):
عَالِمُ الْغَيْبِ فَلَا يُظْهِرُ عَلَىٰ غَيْبِهِ أَحَدًا إِلَّا مَنِ ارْتَضَىٰ مِن رَّسُولٍ
”Mjuzi wa mambo yaliyofichikana na wala hamdhihirishii yeyote ghaibu Yake, isipokuwa yule aliyemridhia ambaye ni Mtume.”[1]
Aliwabashiria (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Maswahabah kumi kuingia Peponi, nao ni: Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan, ´Aliy, Twalhah, az-Zubayr, ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf, Sa´d, Sa´iyd na Abu ´Ubaydah bin al-Jarraah. Vilevile alisema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu Thaabit bin Qays bin Shimaas (Radhiya Allaahu ´anh):
”Hakika ni katika watu wa Peponi.”
Anas bin Maalik amesema:
”Alikuwa anatembea kati yetu na sisi tunasema: ”Hakika yeye ni katika watu wa Peponi.”[2]
[1] 72:26-27
[2] al-Bukhaariy (3613) na Muslim (187).
- Muhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 287-289
- Imechapishwa: 24/12/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)