Kwa vile Hadiyth hii imepokelewa kwa mapokezi mengi (متواتر) na wakaona hawana namna ya kuikwepa, sasa wakataka kujibebetua ili wajikwamue nayo. Wakasema:
“Hushuka”
maana yake ni amri Yake ndio hushuka. Tunawaraddi kwa kuwaambia: katika Hadiyth imekuja ya kwamba Husema: “Ni nani anayeniomba msamaha Nimsamehe? Ni nani anayeniomba Nimpe? Kuna mwenye kutubia Nimkubalie tawbah Yake? Kuna mwenye kuniomba msamaha Nimghufurie? Kuna kwenye kuniomba Nimpe?”[1]
Je, amri inaweza kusema:
“Ni nani anayeniomba Nimpe? Ni nani anayeniomba msamaha Nimsamehe?”
Hili ni batili. Mwenye kusema haya ni Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
Wakasema:
“Hushuka Mola wetu.”
maana yake ni Malaika miongoni mwa Malaika ndiye mwenye kushuka. Tunawaraddi kwa kuwaambia: Je, Malaika ndiye mwenye kusema:
“Ni nani mwenye kuniomba msamaha? Ni nani mwenye kuniomba? Ni nani mwenye kutubia Nimkubalie tawbah yake?”
Hivi kweli Malaika anaweza kusema haya au yanasemwa na Mola (Subhaanahu wa Ta´ala)? Bila shaka ni Mola (Jalla wa ´Alaa).
Kwa hivyo makusudio sio kwamba amri wala Malaika ndiye mwenye kushuka. Kwa kuwa si amri wala Malaika vyote viwili hakuna mwenye kuweza kutamka maneno haya yaliyotajwa katika Hadiyth.
[1] al-Bukhaariy (1145) na Muslim (168) na (758)
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 97-98
- Imechapishwa: 09/01/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)