Tofauti kati ya matarajio na matumaini:
Kutaraji kunakuwa kumeambatana na kujitolea juhudi na mategemezi mazuri. Kuhusu matumaini yanakuwa yameambatana na uzembe. Amesema (Ta´ala):
أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ وَيَرْجُونَ رَحْمَتَهُ وَيَخَافُونَ عَذَابَهُ
“Hao wanaowaomba [wao wenyewe] wanatafuta kwa Mola wao njia [na] kumkurubia kadri wanavyoweza, na wanataraji Rahmah Yake na wanakhofu Adhabu Yake.”[1]
Kutafuta njia ya kumfikia ni kutafuta njia ya kumkurubia kwa mapenzi, ´ibaadah ya kumtii na aina nyenginezo za ´ibaadah[2].
Kwa hiyo ni lazima kwa mtu kuhakikisha matarajio yake. Asiyafungamanishe isipokuwa na Allaah. Asiyafungamanishe na nguvu, kazi yake wala asiyafungamanishe na kiumbe. Miongoni mwa yaliyopokelewa kutoka kwa ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) ni kwamba amesema:
“Mtu asimtarajii mwingine isipokuwa Mola wake na wala asiogope isipokuwa dhambi yake.”[3]
[1] 17:57
[2] Tazama ”Madaarij-us-Saalikiyn” (02/36).
[3] Tazama ”Hilyat-ul-Awliyaa´” (01/76).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 55
- Imechapishwa: 08/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)