Allaah ametofautisha kati ya amri na viumbe Wake; hakuwaita viumbe Wake kuwa amri Yake. Amesema:
أَلَا لَهُ الْخَلْقُ وَالْأَمْرُ
”Tanabahi! Ni Vyake pekee uumbaji na amri.”[1]
Aliposema kuwa viumbe ni Wake, kukaingia viumbe wote. Kisha Akataja ambacho hakikuumbwa na kusema:
وَالْأَمْرُ
”… na amri.”
Amri Yake ndio maneno Yake. Amebarikika Allaah, Mola wa walimwengu, kutokana na maneno Yake kuwa yenye kuumbwa!
Amesemea tena:
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ
“Hakika Sisi tumeiteremsha katika usiku uliobarikiwa – hakika Sisi daima ni Wenye kuonya [watu] – katika [usiku] huo hupambanuliwa kila jambo la hekima.”[2]
Kisha akasema kuhusu Qur-aan:
أَمْرًا مِّنْ عِندِنَا
”… ni amri inayotoka Kwetu.”[3]
Kisha akasema:
لِلَّـهِ الْأَمْرُ مِن قَبْلُ وَمِن بَعْدُ
”Amri ni ya Allaah pekee kabla na baada.”[4]
Bi maana Allaah ndiye Mwenye neno kabla na baada ya kuumba. Allaah anaumba na anaamrisha – na maneno Yake sio uumbaji Wake. Amesema:
ذَٰلِكَ أَمْرُ اللَّـهِ أَنزَلَهُ إِلَيْكُمْ
”Hiyo ni amri ya Allaah amekuteremshieni.”[5]
حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَمْرُنَا وَفَارَ التَّنُّورُ
”… mpaka ilipokuja amri Yetu na maji yakachimbuka kwa nguvu kutoka katika tanuri… ”[6][7]
[1] 7:54
[2] 44:3-4
[3] 44:5
[4] 30:4
[5] 65:5
[6] 11:40
[7] Ibn ´Aqiyl al-Hanbaliy amesema:
”Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ameandika kitabu kinachoitwa ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah waz-Zanaadiqah wal-Qadariyyah.” (al-Aadaab ash-Shar´iyyah (1/274))
Ibn Taymiyyah amesema:
”Kama alivosema Imaam Ahmad katika kitabu chake ”ar-Radd ´alaaz-Zanaadiqah wal-Jahmiyyah.” (Tafsiyr Suurat-il-Ikhlaasw, uk. 239)
Ibn Kathiyr amesema:
”… na hivo ndivo alivosema Ahmad bin Hanbal katika kitabu ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah” (Tafsiyr al-Qur-aan al-´Adhwiym (3/304))
Ibn Hajar al-´Asqalaaniy amesema:
”Amesema waziwazi Ahmad katika kitabu “ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah.” (Fath-ul-Baariy (13/598))
- Muhusika: Imaam Ahmad bin Hanbal (afk. 241)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah waz-Zanaadiqah, uk. 106-107
- Imechapishwa: 22/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)