al-Hasan amesema:
“Kuna sampuli mbili za elimu. Elimu inayokuwa ulimini. Elimu hiyo ni hoja ya Allaah dhidi ya mtu. Elimu inayokuwa moyoni. Hiyo ndio elimu yenye manufaa.”
Salaf walikuwa wakisema:
”Kuna aina tatu ya wanazuoni: mwanachuoni anayemjua Allaah na maamrisho ya Allaah, mwanachuoni anayemjua Allaah lakini si mwenye kujua maamrisho ya Allaah na mwanachuoni anayejua maamrisho ya Allaah lakini hamjui Allaah.”
Mkamilifu wao zaidi ni yule wa kwanza. Naye ni yule anayemcha Allaah na anazitambua hukumu Zake. Shani ni kule mja kuitumia elimu yake kumtambua Mola wake. Anapomtambua Mola wake, basi hakika amempata karibu Naye. Pale atapompata karibu Naye, basi atamkurubia na kuitikia du´aa zake. Imekuja katika upokezi wa ki-israaiyl:
”Mwanadamu! Nitafute utanipata. Ukinipata, basi umepata kila kitu. Na ukinikosa, basi umekosa kila kitu. Na mimi ni Mwenye kupendwa zaidi kwako kuliko kila kitu.”
Dhuun-Nuun alikuwa akiyarudirudi maneno haya usiku:
Jitafutieni kile ambacho
mimi nimekipata
Hakika nimejipatia jengo
isiyokuwa na eneo la nje
Nikijiweka mbali, Ananikuurbia
au nikimkurubia, Anakuwa karibu
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amesema kuhusu Ma´ruuf:
”Anao msingi wa elimu; khofu juu ya Allaah.”
- Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan Fadhwl ´Ilm-is-Salaf ´alaa ´Ilm-il-Khalaf, uk. 77-78
- Imechapishwa: 27/09/2021
al-Hasan amesema:
“Kuna sampuli mbili za elimu. Elimu inayokuwa ulimini. Elimu hiyo ni hoja ya Allaah dhidi ya mtu. Elimu inayokuwa moyoni. Hiyo ndio elimu yenye manufaa.”
Salaf walikuwa wakisema:
”Kuna aina tatu ya wanazuoni: mwanachuoni anayemjua Allaah na maamrisho ya Allaah, mwanachuoni anayemjua Allaah lakini si mwenye kujua maamrisho ya Allaah na mwanachuoni anayejua maamrisho ya Allaah lakini hamjui Allaah.”
Mkamilifu wao zaidi ni yule wa kwanza. Naye ni yule anayemcha Allaah na anazitambua hukumu Zake. Shani ni kule mja kuitumia elimu yake kumtambua Mola wake. Anapomtambua Mola wake, basi hakika amempata karibu Naye. Pale atapompata karibu Naye, basi atamkurubia na kuitikia du´aa zake. Imekuja katika upokezi wa ki-israaiyl:
”Mwanadamu! Nitafute utanipata. Ukinipata, basi umepata kila kitu. Na ukinikosa, basi umekosa kila kitu. Na mimi ni Mwenye kupendwa zaidi kwako kuliko kila kitu.”
Dhuun-Nuun alikuwa akiyarudirudi maneno haya usiku:
Jitafutieni kile ambacho
mimi nimekipata
Hakika nimejipatia jengo
isiyokuwa na eneo la nje
Nikijiweka mbali, Ananikuurbia
au nikimkurubia, Anakuwa karibu
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amesema kuhusu Ma´ruuf:
”Anao msingi wa elimu; khofu juu ya Allaah.”
Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Bayaan Fadhwl ´Ilm-is-Salaf ´alaa ´Ilm-il-Khalaf, uk. 77-78
Imechapishwa: 27/09/2021
https://firqatunnajia.com/26-msingi-wa-elimu-khofu-juu-ya-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)