Kuna aina mbili ya maamrisho:
1 – Miongoni mwa mambo aliyoamrisha Allaah kwa njia ya ulazima ni kama kusimamisha swalah. Amesema (Ta´ala):
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ
“Simamisheni swalah.”[1]
Kwa hivyo hiajuzu kumtekelezea swalah mwingine asiyekuwa Allaah. Mtu akimswalia asiyekuwa Allaah amefanya shirki.
Miongoni mwa mambo aliyoamrisha Allaah kwa njia ya mapendekezo ni kutumia Siwaak. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Lau nisingechelea kuwatia uzito ummah wangu basi ningewaamrisha kutumia Siwaak wakati wa kila swalah.”[2]
Siwaak ni ´ibaadah inayopendeza. Mtu anatumia Siwaak hali ya kumwabudu Allaah. Kwa hivyo mtu asitumie Siwaak hali ya kuabudu kwa mwingine asiyekuwa Allaah.
[1] 02:43
[2] al-Bukhaariy (887) na Muslim (252).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 44
- Imechapishwa: 06/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)