43 – al-Fadhwl bin al-Muqaatil ametuhadithia: ´Abdullaah bin Ibraahiym bin ´Umar bin Kaysaan ametuhadithia, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema:
”Ibn Abiy Najiyh aliikaa kwa muda wa miaka thelathini bila ya kusema neno la kumuudhi yule mwenye kutangamana naye.”
44 – Muhammad bin Sallaam ametuhadithia, kutoka kwa Ibn ´Uyaynah, ambaye amesema:
”Mnajua ni nini amani? Amani ni wewe uwe na amani nami na usalimike nami.”
45 – Nimemsikia Abu ´Abdillaah al-Musnadiy akisema:
”Silm bin Saalim alienda kwa Ibn ´Uyaynah (Rahimahu Allaah) na akawa anamuhadithia namna amefanya kadhaa na kadhaa. Ibn ´Uyaynah akamtazama na kusema: ”Akili yako imenishauri dawa. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ
“… na jiepushe na wajinga.”[1]
46 – Ibraahiym bin Muusa ametuhadithia: Ibn Abiy Zaa-idah amenikhabarisha: Baba yangu amenikhabarisha, kutoka kwa Khaalid bin Salamah, kutoka kwa al-Bahiy, kutoka kwa ´Urwah, kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia:
”Simama ujipiganie.”
47 – Musaddad ametuhadithia: Yahyaa bin Sa´iyd ametuhadithia, kutoka kwa Thawr: Habiyb bin ´Ubayd amenihadithia, kutoka kwa al-Miqdaam bin Ma´diy Karib, ambaye alikutana naye, ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Akimpenda mmoja wenu ndugu yake basi amjuze kuwa anampenda.”
48 – Nimemsikia Muusa bin Ismaa´iyl akisema: Nimemsikia Abu ´Aaswim akisema:
”Sijapatapo kumsengenya mtu tangu nilipojifunza kuwa usengenyi unawadhuru wenye nao.”
49 – Musaddad ametuhadithia: Ismaa´iyl bin Ibraahiym ametuhadithia: Ziyaad bin Mikhraaq ametuhadithia, kutoka kwa Mu´aawiyah bin Qurrah, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema:
”Bwana mmoja alisema: ”Mimi humchinja kondoo na huku namuonea huruma.” Au alisema: ”Mimi namuhurumia kondoo kumchinja.” Ndipo akasema: ”Ukimuhurumia kondoo nawe Allaah anakuonea huruma mara mbili.”
[1] 7:199
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Ismaa´iyl al-Bukhaariy (a.f.k 256)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Birr-ul-Waalidayn, uk. 140-146
- Imechapishwa: 20/01/2025
43 – al-Fadhwl bin al-Muqaatil ametuhadithia: ´Abdullaah bin Ibraahiym bin ´Umar bin Kaysaan ametuhadithia, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema:
”Ibn Abiy Najiyh aliikaa kwa muda wa miaka thelathini bila ya kusema neno la kumuudhi yule mwenye kutangamana naye.”
44 – Muhammad bin Sallaam ametuhadithia, kutoka kwa Ibn ´Uyaynah, ambaye amesema:
”Mnajua ni nini amani? Amani ni wewe uwe na amani nami na usalimike nami.”
45 – Nimemsikia Abu ´Abdillaah al-Musnadiy akisema:
”Silm bin Saalim alienda kwa Ibn ´Uyaynah (Rahimahu Allaah) na akawa anamuhadithia namna amefanya kadhaa na kadhaa. Ibn ´Uyaynah akamtazama na kusema: ”Akili yako imenishauri dawa. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ
“… na jiepushe na wajinga.”[1]
46 – Ibraahiym bin Muusa ametuhadithia: Ibn Abiy Zaa-idah amenikhabarisha: Baba yangu amenikhabarisha, kutoka kwa Khaalid bin Salamah, kutoka kwa al-Bahiy, kutoka kwa ´Urwah, kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia:
”Simama ujipiganie.”
47 – Musaddad ametuhadithia: Yahyaa bin Sa´iyd ametuhadithia, kutoka kwa Thawr: Habiyb bin ´Ubayd amenihadithia, kutoka kwa al-Miqdaam bin Ma´diy Karib, ambaye alikutana naye, ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Akimpenda mmoja wenu ndugu yake basi amjuze kuwa anampenda.”
48 – Nimemsikia Muusa bin Ismaa´iyl akisema: Nimemsikia Abu ´Aaswim akisema:
”Sijapatapo kumsengenya mtu tangu nilipojifunza kuwa usengenyi unawadhuru wenye nao.”
49 – Musaddad ametuhadithia: Ismaa´iyl bin Ibraahiym ametuhadithia: Ziyaad bin Mikhraaq ametuhadithia, kutoka kwa Mu´aawiyah bin Qurrah, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema:
”Bwana mmoja alisema: ”Mimi humchinja kondoo na huku namuonea huruma.” Au alisema: ”Mimi namuhurumia kondoo kumchinja.” Ndipo akasema: ”Ukimuhurumia kondoo nawe Allaah anakuonea huruma mara mbili.”
[1] 7:199
Muhusika: Imaam Muhammad bin Ismaa´iyl al-Bukhaariy (a.f.k 256)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Birr-ul-Waalidayn, uk. 140-146
Imechapishwa: 20/01/2025
https://firqatunnajia.com/24-kumuhurumia-kondoo/