50 – Ibraahiym bin al-Mundhir ametuhadithia: Ma´n ametuhadithia, kutoka kwa Mu´aawiyah, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin Jubayr, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Nawwaas bin Swam´aan al-Answaariy ambaye ameeleza kwamba:
”Nilimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya wema na dhambi. Akasema: ”Wema ni tabia njema, na dhambi ni yale yanayokukereketa nafsini mwako na ukachelea watu wasije kuyajua.”
51 – Abul-Yamaan ametuhadithia: Shu´ayb ametukhabarisha, kutoka kwa az-Zuhriy: Saalim amenihadithia, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema: Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema juu ya mimbari:
”Hapana shaka kwamba fitina itatokea hapa, ambapo kutazuka pembe ya shaytwaan.”
Akaashiria Magharibi.
52 – ´Abdullaah bin Swaalih ametuhadithia: al-Layth amenihadithia: ´Uqayl amenihadithia, kutoka kwa Ibn Shihaab, Saalim bin ´Abdillaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhum) amenikhabarisha, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisimama akiwakhutubia watu na akasema: ”Fitina itatokea hapa, ambapo kutazuka pembe ya shaytwaan.” Bi maana Mashariki.”
53 – al-Humaydiy ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia: Muhammad bin ´Amr bin ´Alqamah ametuhadithia, kutoka kwa Yahyaa bin ´Abdir-Rahmaan bin Haatwib, kutoka kwa ´Abdullaah bin az-Zubayr: az-Zubayr amesema:
”Wakati kuliposhuka:
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
”Halafu hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenu mtazozana.”[1]
az-Zubayr alisema: ”Ee Mtume wa Allaah! Tutazozana, baada ya mizozo tuliokuwa nayo duniani?” Akasema: ”Ndio.” Ndipo nikasema: ”Mambo ni mazito.”
54 – Muhammad bin ´Ubaydillaah Abu Thaabit al-Madaniy ametuhadithia: ´Umar bin Twalhah al-Waqqaasiy ametuhadithia, kutoka kwa Muhammad bin ´Amr, kutoka kwa Yahyaa bin ´Abdir-Rahmaan: Nimemsikia ´Abdullaah bin az-Zubayr akisema:
”Wakati kuliposhuka:
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
”Halafu hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenu mtazozana.”
az-Zubayr alisema: ”Ee Mtume wa Allaah! Je, yale madhambi tuliyofanya duniani yatakaririwa?” Akasema: ”Ndio.” Yatakaririwa kwenu, mpaka kila mwenye haki apewe haki yake.” az-Zubayr (Radhiya Allaahu ´anh) akasema: ”Naapa kwa Allaah! Mambo ni mazito.”
Hammaad bin Salamah amepokea mfano wa hayo, kutoka kwa Habiyb, kutoka kwa al-Hasan: az-Zubayr amesema… Shaddaad bin Sa´iyd amepokea mfano wa hayo, kutoka kwa Ghaylaan, kutoka kwa Mutwarrif: az-Zubayr amesema… Matamshi yao ni yenye kukaribiana. Hata hivyo ile ya kwanza ndio Hadiyth Swahiyh zaidi.
55 – Abur-Rabiy´ Sulaymaan bin Daawuud ametuhadithia: Ya´quub al-Qummiy ametuhadithia: Ja´far – Ibn Abiyl-Mughiyrah – ametuhadithia, kutoka kwa Sa´iyd bin Jubayr, kutoka kwa Ibn ´Umar, ambaye amesema:
”Wakati kuliposhuka:
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
”Halafu hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenu mtazozana.”
hatukujua tafsiri yake. Wakati kulipotokea fitina, tukasema: ”Haya ndio yale ambayo Mola wetu ametuahidi kuzozana kwayo.”
[1] 39:31
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Ismaa´iyl al-Bukhaariy (a.f.k 256)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Birr-ul-Waalidayn, uk. 146-150
- Imechapishwa: 20/01/2025
50 – Ibraahiym bin al-Mundhir ametuhadithia: Ma´n ametuhadithia, kutoka kwa Mu´aawiyah, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin Jubayr, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Nawwaas bin Swam´aan al-Answaariy ambaye ameeleza kwamba:
”Nilimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya wema na dhambi. Akasema: ”Wema ni tabia njema, na dhambi ni yale yanayokukereketa nafsini mwako na ukachelea watu wasije kuyajua.”
51 – Abul-Yamaan ametuhadithia: Shu´ayb ametukhabarisha, kutoka kwa az-Zuhriy: Saalim amenihadithia, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema: Nimemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema juu ya mimbari:
”Hapana shaka kwamba fitina itatokea hapa, ambapo kutazuka pembe ya shaytwaan.”
Akaashiria Magharibi.
52 – ´Abdullaah bin Swaalih ametuhadithia: al-Layth amenihadithia: ´Uqayl amenihadithia, kutoka kwa Ibn Shihaab, Saalim bin ´Abdillaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhum) amenikhabarisha, kutoka kwa baba yake, ambaye amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisimama akiwakhutubia watu na akasema: ”Fitina itatokea hapa, ambapo kutazuka pembe ya shaytwaan.” Bi maana Mashariki.”
53 – al-Humaydiy ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia: Muhammad bin ´Amr bin ´Alqamah ametuhadithia, kutoka kwa Yahyaa bin ´Abdir-Rahmaan bin Haatwib, kutoka kwa ´Abdullaah bin az-Zubayr: az-Zubayr amesema:
”Wakati kuliposhuka:
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
”Halafu hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenu mtazozana.”[1]
az-Zubayr alisema: ”Ee Mtume wa Allaah! Tutazozana, baada ya mizozo tuliokuwa nayo duniani?” Akasema: ”Ndio.” Ndipo nikasema: ”Mambo ni mazito.”
54 – Muhammad bin ´Ubaydillaah Abu Thaabit al-Madaniy ametuhadithia: ´Umar bin Twalhah al-Waqqaasiy ametuhadithia, kutoka kwa Muhammad bin ´Amr, kutoka kwa Yahyaa bin ´Abdir-Rahmaan: Nimemsikia ´Abdullaah bin az-Zubayr akisema:
”Wakati kuliposhuka:
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
”Halafu hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenu mtazozana.”
az-Zubayr alisema: ”Ee Mtume wa Allaah! Je, yale madhambi tuliyofanya duniani yatakaririwa?” Akasema: ”Ndio.” Yatakaririwa kwenu, mpaka kila mwenye haki apewe haki yake.” az-Zubayr (Radhiya Allaahu ´anh) akasema: ”Naapa kwa Allaah! Mambo ni mazito.”
Hammaad bin Salamah amepokea mfano wa hayo, kutoka kwa Habiyb, kutoka kwa al-Hasan: az-Zubayr amesema… Shaddaad bin Sa´iyd amepokea mfano wa hayo, kutoka kwa Ghaylaan, kutoka kwa Mutwarrif: az-Zubayr amesema… Matamshi yao ni yenye kukaribiana. Hata hivyo ile ya kwanza ndio Hadiyth Swahiyh zaidi.
55 – Abur-Rabiy´ Sulaymaan bin Daawuud ametuhadithia: Ya´quub al-Qummiy ametuhadithia: Ja´far – Ibn Abiyl-Mughiyrah – ametuhadithia, kutoka kwa Sa´iyd bin Jubayr, kutoka kwa Ibn ´Umar, ambaye amesema:
”Wakati kuliposhuka:
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عِندَ رَبِّكُمْ تَخْتَصِمُونَ
”Halafu hakika nyinyi siku ya Qiyaamah mbele ya Mola wenu mtazozana.”
hatukujua tafsiri yake. Wakati kulipotokea fitina, tukasema: ”Haya ndio yale ambayo Mola wetu ametuahidi kuzozana kwayo.”
[1] 39:31
Muhusika: Imaam Muhammad bin Ismaa´iyl al-Bukhaariy (a.f.k 256)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Birr-ul-Waalidayn, uk. 146-150
Imechapishwa: 20/01/2025
https://firqatunnajia.com/25-mizozo-siku-ya-qiyaamah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)