Swali: Kuhusu Witr ya Tarawiyh mwishoni mwa Ramadhaan. Je, niswali Witr na nilale au niicheleweshe pamoja na kisimamo cha mwishoni mwa usiku kwa sababu mimi hulala kati ya muda wa Tarawiyh na kisimamo cha usiku?
Jibu: Ukiswali na imamu swalah ya Tarawiyh basi bora ni wewe kuswali Witr pamoja naye ili upate ujira kamilifu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayesimama pamoja na imamu mpaka akamaliza basi anaandikiwa kuwa ameswali usiku mzima.”[1]
Ukiamka mwishoni mwa usiku na ukataka kuswali basi swali kile kitachokuwa wepesi kwako pasi na Witr. Kwa sababu hakuna Witr mbili katika usiku mmoja kama ilivyokwishatangulia. Ukiacha Witr mwanzoni mwa usiku au Witr ukaifanya shufwa kwa kuongeza Rak´ah moja mwanzoni au mwishoni mwa usiku ili uweze kuswali Witr mwishoni mwa usiku ni sawa pia.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh
Bakr Abu Zayd
[1] Abu Daawuud na at-Tirmidhiy.
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Swalaat-it-Taraawiyh, uk. 25-26
- Imechapishwa: 15/04/2022
Swali: Kuhusu Witr ya Tarawiyh mwishoni mwa Ramadhaan. Je, niswali Witr na nilale au niicheleweshe pamoja na kisimamo cha mwishoni mwa usiku kwa sababu mimi hulala kati ya muda wa Tarawiyh na kisimamo cha usiku?
Jibu: Ukiswali na imamu swalah ya Tarawiyh basi bora ni wewe kuswali Witr pamoja naye ili upate ujira kamilifu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayesimama pamoja na imamu mpaka akamaliza basi anaandikiwa kuwa ameswali usiku mzima.”[1]
Ukiamka mwishoni mwa usiku na ukataka kuswali basi swali kile kitachokuwa wepesi kwako pasi na Witr. Kwa sababu hakuna Witr mbili katika usiku mmoja kama ilivyokwishatangulia. Ukiacha Witr mwanzoni mwa usiku au Witr ukaifanya shufwa kwa kuongeza Rak´ah moja mwanzoni au mwishoni mwa usiku ili uweze kuswali Witr mwishoni mwa usiku ni sawa pia.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah bin Ghudayyaan
Swaalih al-Fawzaan
´Abdul-´Aziyz Aalish-Shaykh
Bakr Abu Zayd
[1] Abu Daawuud na at-Tirmidhiy.
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Swalaat-it-Taraawiyh, uk. 25-26
Imechapishwa: 15/04/2022
https://firqatunnajia.com/23-witr-ya-tarawiyh-mwishoni-mwa-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)