Imaam Ibn Abiy Daawuud (Rahimahu Allaah) amesema:
ولا تقل القرآن خلْقٌ قرأْتُهُ
05 – Wala usiseme kuwa kisomo cha Qur-aan kimeumbwa
فإن كلام اللهِ باللفظ يُوضحُ
kwani hakika maneno ya Allaah yanawekwa wazi kwa matamshi
MAELEZO
Haya ni madhehebu ya tatu katika masuala haya.
1 – Wanasema wazi kuwa Qur-aan ni kiumbe.
2 – Wanasimama. Bi maana hawasemi kuwa imeumbwa wala haikuumbwa.
3 – Matamshi ya Qur-aan ni kiumbe. Mtu anasema kuwa matamshi yake ya Qur-aan yameumbwa. Hii ni njama ya kusema kuwa Qur-aan imeumbwa. Haijuzu kwako kusema kuwa matamshi yako ya Qur-aan yameumbwa na wala haijuzu vilevile kusema kuwa matamshi yako ya Qur-aan hayakuumbwa. Ni lazima upambanue. Kwa sababu ukisema kwamba matamshi yako ya Qur-aan ni kiumbe na usipambanue, hii ni ´Aqiydah ya Jahmiyyah. Vilevile ukisema kuwa matamshi yako ya Qur-aan sio kiumbe, huku ni kuwasapoti ´Aqiydah ya Jahmiyyah. Kwa kuwa ukisema kwamba matamshi yako ya Qur-aan hayakuumbwa, utakuwa umeingiza matendo yako pamoja na matendo ya Allaah na umefanya kitendo chako hakikuumbwa. Hii ni ´Aqiydah ya Qadariyyah ambao wanapinga makadirio na wanaona kuwa viumbe ndio wanaovumbua na kuumba matendo yao wenyewe.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 75
- Imechapishwa: 02/01/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)