21. Ilikuweje yake Mtume na wale wafuasi wake waliomwamini baada ya kudhihirisha ulingano?

Swali 21: Ilikuweje hali yake yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wale wafuasi wake waliomwamini baada ya kudhihirisha ulingano?

Jibu: Wakati alipodhihirisha (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ulingano basi washirikina walizidi katika kumuudhi na kuwaudhi waislamu. Hali iliendelea hivo mpaka wakapewa idhini ya kuhajiri Uhabeshi kwa an-Najaashiy. Wakahajiri takriban watu 80, baadhi wakiwa wenyewe, wengine pamoja na familia zao.

  • Mhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 97
  • Imechapishwa: 17/09/2023