Swali 21: Ilikuweje hali yake yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wale wafuasi wake waliomwamini baada ya kudhihirisha ulingano?
Jibu: Wakati alipodhihirisha (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ulingano basi washirikina walizidi katika kumuudhi na kuwaudhi waislamu. Hali iliendelea hivo mpaka wakapewa idhini ya kuhajiri Uhabeshi kwa an-Najaashiy. Wakahajiri takriban watu 80, baadhi wakiwa wenyewe, wengine pamoja na familia zao.
- Muhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 97
- Imechapishwa: 17/09/2023