Mtunzi amesema:
“Dalili ya kupangilia.”
Ni kwamba Allaah (Ta´ala) katika Aayah inayozungumzia wudhuu´ ameingiza viungo vinavyooshwa baina ya maosho, kama tulivyotangulia kusema.
Mtunzi amesema:
Dalili ya kupangilia ni Hadiyth:
“Anza kwa Alichoanza nacho Allaah.”[1]
imetupa faida juu ya ulazima wa kutawadha kwa kupangilia, kama alivotaja Allaah.
Maneno yake mtunzi:
“Na dalili ya Muwaalaah ni Hadiyth ya mtu aliyeacha sehemu bila ya kuosha. Imepokelewa kwamba wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliona mtu aliyeacha sehemu katika mguu wake kiasi cha dirhamu hakikufikiwa na maji, hivyo akamuamrisha (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kurudia na kutia wudhuu´ upya. Khaalid amepokea kutoka kwa baadhi ya Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mtume alimwona bwana mmoja akiswali na nyuma ya mgongo wake kuna kiasi cha dirhamu hakikufikiwa na maji. Basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwamrisha arudi kutawadha na kuswali.”
Endapo Muwaalaah ingekuwa sio lazima basi ingelitosha kuosha sehemu ile peke yake.
[1] an-Nasaa’iy (2962). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Tamaam-ul-Minnah”, uk. 88.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 31-32
- Imechapishwa: 15/12/2021
Mtunzi amesema:
“Dalili ya kupangilia.”
Ni kwamba Allaah (Ta´ala) katika Aayah inayozungumzia wudhuu´ ameingiza viungo vinavyooshwa baina ya maosho, kama tulivyotangulia kusema.
Mtunzi amesema:
Dalili ya kupangilia ni Hadiyth:
“Anza kwa Alichoanza nacho Allaah.”[1]
imetupa faida juu ya ulazima wa kutawadha kwa kupangilia, kama alivotaja Allaah.
Maneno yake mtunzi:
“Na dalili ya Muwaalaah ni Hadiyth ya mtu aliyeacha sehemu bila ya kuosha. Imepokelewa kwamba wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliona mtu aliyeacha sehemu katika mguu wake kiasi cha dirhamu hakikufikiwa na maji, hivyo akamuamrisha (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kurudia na kutia wudhuu´ upya. Khaalid amepokea kutoka kwa baadhi ya Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mtume alimwona bwana mmoja akiswali na nyuma ya mgongo wake kuna kiasi cha dirhamu hakikufikiwa na maji. Basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwamrisha arudi kutawadha na kuswali.”
Endapo Muwaalaah ingekuwa sio lazima basi ingelitosha kuosha sehemu ile peke yake.
[1] an-Nasaa’iy (2962). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Tamaam-ul-Minnah”, uk. 88.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 31-32
Imechapishwa: 15/12/2021
https://firqatunnajia.com/21-dalili-juu-ya-ulazima-kupangilia-na-muwaalaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)