Swali: Ni du´aa ipi inayotakiwa kusomwa wakati wa kukata swawm? Mtu afungue swawm kwa kitu gani?
Jibu: Du´aa inayotakiwa kusomwa wakati wa kukata swawm:
ذَهَبَ الظَّمَأُ وَابْتَلَّتِ الْعُرُوقُ وَثَبَتَ الْأَجْرُ إِنْ شَاءَ اللَّهُ
“Kiu kimeondoka, mishipa imerowana na ujira umepatikana – Allaah akitaka.”[1]
Mfungaji atafungua kwa tende tosa au tende za kawaida. Akikosa basi atafungua kwa maji, hivyo ndivo katukhabarisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Abu Daawuud (2357), al-Bayhaqiy katika ”as-Sunan al-Kubraa” (4/239) na katika ”as-Sunan as-Sughraa” (1390) na ad-Daaraqutwniy (240). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Irwaa’-ul-Ghaliyl”.
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 22
- Imechapishwa: 21/03/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket