Swali: Kuna du´aa gani iliyopendekezwa wakati wa kukata swawm? Mtu aseme:
ذَهَبَ الظَّمَأُ وَابْتَلَّتِ الْعُرُوقُ وَثَبَتَ الْأَجْرُ إِنْ شَاءَ اللَّهُ
“Kiu kimeondoka, mishipa imerowana na ujira umepatikana – Allaah akitaka.”[1]?
Jibu: Imepokelewa kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema wakati alipokata swawm:
ذَهَبَ الظَّمَأُ وَابْتَلَّتِ الْعُرُوقُ وَثَبَتَ الْأَجْرُ إِنْ شَاءَ اللَّهُ
“Kiu kimeondoka, mishipa imerowana na ujira umepatikana – Allaah akitaka.”
Kumepokelewa vilevile:
اللَّهُمَّ لَكَ صُمْتُ وَعَلَى رِزْقِكَ أَفْطَرْتُ
“Ee Allaah! Nimefunga kwa ajili yako na nimefutari kwa riziki yako.”[2]
Kwa hali yoyote kuna uwezekano mkubwa wa kuitikiwa du´aa wakati wa kukata swawm. Kwa hiyo muislamu anatakiwa kuangalia du´aa zenye manufaa na zenye kuenea na aombe kwazo kwa kutaraji kuitikiwa na kupata thawabu za Allaah.
[1] Abu Daawuud (2357), al-Bayhaqiy katika ”as-Sunan al-Kubraa” (4/239) na katika ”as-Sunan as-Sughraa” (1390) na ad-Daaraqutwniy (240). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Irwaa’-ul-Ghaliyl”.
[2] Abu Daawuud (2358), ad-Daaraqutwniy (240) na Ibn-us-Sunniy katika ”´Amal-ul-Yawm wal-Laylah” (482). Ibn-ul-Qayyim amesema:
”Haikuthibiti.” (Zaad-ul-Ma´aad (2/51))
Ibn Hajar amesema:
”Cheni ya wapokezi ni dhaifu.” (Talkhiysw-ul-Habiyr)
Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf Sunan al-Albaaniy” (2358).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 22
- Imechapishwa: 21/03/2022
Swali: Kuna du´aa gani iliyopendekezwa wakati wa kukata swawm? Mtu aseme:
ذَهَبَ الظَّمَأُ وَابْتَلَّتِ الْعُرُوقُ وَثَبَتَ الْأَجْرُ إِنْ شَاءَ اللَّهُ
“Kiu kimeondoka, mishipa imerowana na ujira umepatikana – Allaah akitaka.”[1]?
Jibu: Imepokelewa kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema wakati alipokata swawm:
ذَهَبَ الظَّمَأُ وَابْتَلَّتِ الْعُرُوقُ وَثَبَتَ الْأَجْرُ إِنْ شَاءَ اللَّهُ
“Kiu kimeondoka, mishipa imerowana na ujira umepatikana – Allaah akitaka.”
Kumepokelewa vilevile:
اللَّهُمَّ لَكَ صُمْتُ وَعَلَى رِزْقِكَ أَفْطَرْتُ
“Ee Allaah! Nimefunga kwa ajili yako na nimefutari kwa riziki yako.”[2]
Kwa hali yoyote kuna uwezekano mkubwa wa kuitikiwa du´aa wakati wa kukata swawm. Kwa hiyo muislamu anatakiwa kuangalia du´aa zenye manufaa na zenye kuenea na aombe kwazo kwa kutaraji kuitikiwa na kupata thawabu za Allaah.
[1] Abu Daawuud (2357), al-Bayhaqiy katika ”as-Sunan al-Kubraa” (4/239) na katika ”as-Sunan as-Sughraa” (1390) na ad-Daaraqutwniy (240). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Irwaa’-ul-Ghaliyl”.
[2] Abu Daawuud (2358), ad-Daaraqutwniy (240) na Ibn-us-Sunniy katika ”´Amal-ul-Yawm wal-Laylah” (482). Ibn-ul-Qayyim amesema:
”Haikuthibiti.” (Zaad-ul-Ma´aad (2/51))
Ibn Hajar amesema:
”Cheni ya wapokezi ni dhaifu.” (Talkhiysw-ul-Habiyr)
Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf Sunan al-Albaaniy” (2358).
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 22
Imechapishwa: 21/03/2022
https://firqatunnajia.com/17-duaa-wakati-wa-kukata-swawm/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)