17. Hadiyth “Yule mwenye kuswali Subh basi yuko katika ulinzi wa Allaah… “

367 – Jundub bin ´Abdillaah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

مَن صلّى الصبحَ فهو في ذِمَّةِ اللهِ، فلا يَطلبنَّكم اللهُ من ذِمَّتِه بشيءٍ، فإنَّه من يَطْلُبْهُ من ذِمته بشيء يُدركْه، ثم يُكِيَّه على وجهه في نارِ جَهنَّم

“Yule mwenye kuswali Subh basi yuko katika ulinzi wa Allaah. Hivyo basi, msifanye Allaah akakutakeni kitu kwa ulinzi Wake. Kwa sababu Atakayemtaka kitu kwa ulinzi Wake, basi atamdiriki kisha atamtupa kwa uso wake katika Moto wa Jahannam.”[1]

Ameipokea Muslim, na tamko ni lake, Abu Daawuud[2], at-Tirmidhiy na wengineo.

[1] Swahiyh.

[2] Imekuja namna hii katika ile ya asili, lakini Hadiyth haiko kabisa kwa Abu Daawuud, kama nilivyobainisha katika “as-Swahiyhah” (2890). 

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/270)
  • Imechapishwa: 25/08/2023
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy