16- Alipokuwa anaswali (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), alikuwa akiinamisha kichwa chake na akiangalia ardhini[1].
Alipoingia Ka´bah macho yake hayakuacha mahala anaposujudia mpaka alipotoka[2].
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Nyumbani hakutakiwi kuwa kitu kinachomshughulisha mswaliji.”[3]
Amekataza mtu kutazama mbinguni[4].
Amesisitiza makatazo na kusema:
“Waache wale wanaonyanyua macho yao juu katika swalah au hayatowarudilia.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“… au wayakose.”[5]
Katika Hadiyth nyingine imekuja:
“Mnaposwali msiangaze, kwani hakika Allaah anauelekeza uso Wake mbele ya uso wa mja Wake maadamu haangazi kwengine.”[6]
Amesema vilevile kuhusu kuangaza huku na kule:
“Ni unyakuaji ambao shaytwaan ananyakua swalah ya mja.”[7]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Allaah haachi kuwa mbele ya yule mwenye kuswali midhali haangazi huku na kule. Anapougeuza uso wake Anaondoka kutoka kwake.”[8]
Amekataza mambo matatu; kudonoa kama anavyodonoa jogoo, kukaa kama anavyokaa mbwa na kuangaza kama mbweha[9].
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swali swalah ya kuaga kama vile unamuona. Ikiwa wewe humuoni, basi Yeye anakuona.”[10]
Amesema pia:
“Hakuna mtu anayeswali swalah ya faradhi pindi wakati wake unapoingia, akatawadha vizuri, akawa na unyenyekevu na kurukuu´ vizuri, isipokuwa inakuwa ni kafara ya madhambi yake yaliyotangulia isipokuwa yale makubwa – hili linahusu mwaka mzima.” Muslim.
Aliswali (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwenye Khamiyswah[11] iliyo na mifumo na akatazama mifumo yake. Alipomaliza akasema:
“Ipelekeni kanzu hii kwa Abu Jahm na mniletee Anbajaaniyah[12] ya Abu Jahm. Inanishughulisha kutokamana na swalah yangu.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Kwani nimetazama mifumo yake katika swalah na imekaribia kunitia katika mtihani.”[13]
´Aaishah alikuwa na kitambaa cha mapicha kilichotandazwa mpaka kwenye Sahwah[14] ambacho Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali kukielekea. Kisha akasema:
“Kiondoeni kwangu [kwani kila mara ninaona mapicha yake mbele yangu ninaposwali].”[15]
Alikuwa akisema:
“Kusiswaliwe pindi chakula kimeshatengwa au pindi mtu anapohitajia kufanya haja mbili.”[16]
[1] al-Bayhaqiy na al-Haakim aliyesema kuwa ni Swahiyh, na ni kweli. Hadiyth hii ina upokezi unaoitilia nguvu kutoka kwa Maswahabah kumi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na imepokelewa na Ibn ´Asaakir (17/202/2). Tazama””al-Irwaa’” (354).
[2] al-Bayhaqiy na al-Haakim aliyesema kuwa ni Swahiyh, na ni kweli.
[3] Abuu Daawuud na Ahmad kwa isnadi Swahiyh.
[4] al-Bukhaariy na Abuu Daawuud.
[5] al-Bukhaariy, Muslim na as-Siraaj.
[6] at-Tirmidhiy na al-Haakim aliyesema kuwa ni Swahiyh. Swahiyh at-Targhiyb (353).
[7] al-Bukhaariy na Abuu Daawuud.
[8] Abuu Daawuud na wengineo. Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan. Swahiyh at-Targhiyb (555).
[9] Ahmad na Abuu Ya´laa. (Swahiyh at-Targhiyb (556).
[10] al-Mukhallasw i ”Ahaadiyth Muntaqaat, at-Twabaraaniy, ar-Rawayaaniy, adh-Dhwiyaa’, Ibn Maajah, Ahmad na Ibn ´Asaakir. Swahiyh kwa mujibu wa Faqiyh al-Haythamiy katika “Asnaa al-Matwaalib””.
[11] Nguo ya pamba iliyofumwa.
[12] Nguo pana ambayo haikufumwa.
[13] al-Bukhaariy, Muslim na Maalik. Imetajwa katika ”al-Irwaa’”’” (376).
[14] Kijumba kidogo kilichofukiwa kidogo ardhini na kimeshabihiana na chumba cha kulalia au chumba cha kuhifadhia vitu. (an-Nihaayah)
[15] al-Bukhaariy, Muslim na Abuu ´Awaanah. Sababu – na Allaah ndiye mwenye kujua zaidi – ya ni kwa nini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuamrisha mapicha yachanwe na badala yake akatosheka na kuyaondo, ni kwa sababu hayakuwa na roho. Dalili ya hilo ni kwamba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyachana mapicha mengine, kama ilivyotajwa katika mapokezi katika al-Bukhaariy na Muslim. Anayetaka kutafiti haya zaidi arejee katika “Fath-ul-Baariy” (10/321) na ”Ghaayat-ul-Maraam fiy Takhriyj Ahaadiyth al-Halaal wal-Haraam ”(131-145).
[16] al-Bukhaariy na Muslim ilihali hiyo Hadiyth nyingne inamwendea Ibn Abiy Shaybah (12/110/2). Imetajwa katika ”al-Irwaa’” (8).
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 78-80
- Imechapishwa: 13/10/2016
16- Alipokuwa anaswali (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), alikuwa akiinamisha kichwa chake na akiangalia ardhini[1].
Alipoingia Ka´bah macho yake hayakuacha mahala anaposujudia mpaka alipotoka[2].
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Nyumbani hakutakiwi kuwa kitu kinachomshughulisha mswaliji.”[3]
Amekataza mtu kutazama mbinguni[4].
Amesisitiza makatazo na kusema:
“Waache wale wanaonyanyua macho yao juu katika swalah au hayatowarudilia.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“… au wayakose.”[5]
Katika Hadiyth nyingine imekuja:
“Mnaposwali msiangaze, kwani hakika Allaah anauelekeza uso Wake mbele ya uso wa mja Wake maadamu haangazi kwengine.”[6]
Amesema vilevile kuhusu kuangaza huku na kule:
“Ni unyakuaji ambao shaytwaan ananyakua swalah ya mja.”[7]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Allaah haachi kuwa mbele ya yule mwenye kuswali midhali haangazi huku na kule. Anapougeuza uso wake Anaondoka kutoka kwake.”[8]
Amekataza mambo matatu; kudonoa kama anavyodonoa jogoo, kukaa kama anavyokaa mbwa na kuangaza kama mbweha[9].
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swali swalah ya kuaga kama vile unamuona. Ikiwa wewe humuoni, basi Yeye anakuona.”[10]
Amesema pia:
“Hakuna mtu anayeswali swalah ya faradhi pindi wakati wake unapoingia, akatawadha vizuri, akawa na unyenyekevu na kurukuu´ vizuri, isipokuwa inakuwa ni kafara ya madhambi yake yaliyotangulia isipokuwa yale makubwa – hili linahusu mwaka mzima.” Muslim.
Aliswali (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwenye Khamiyswah[11] iliyo na mifumo na akatazama mifumo yake. Alipomaliza akasema:
“Ipelekeni kanzu hii kwa Abu Jahm na mniletee Anbajaaniyah[12] ya Abu Jahm. Inanishughulisha kutokamana na swalah yangu.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Kwani nimetazama mifumo yake katika swalah na imekaribia kunitia katika mtihani.”[13]
´Aaishah alikuwa na kitambaa cha mapicha kilichotandazwa mpaka kwenye Sahwah[14] ambacho Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali kukielekea. Kisha akasema:
“Kiondoeni kwangu [kwani kila mara ninaona mapicha yake mbele yangu ninaposwali].”[15]
Alikuwa akisema:
“Kusiswaliwe pindi chakula kimeshatengwa au pindi mtu anapohitajia kufanya haja mbili.”[16]
[1] al-Bayhaqiy na al-Haakim aliyesema kuwa ni Swahiyh, na ni kweli. Hadiyth hii ina upokezi unaoitilia nguvu kutoka kwa Maswahabah kumi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na imepokelewa na Ibn ´Asaakir (17/202/2). Tazama””al-Irwaa’” (354).
[2] al-Bayhaqiy na al-Haakim aliyesema kuwa ni Swahiyh, na ni kweli.
[3] Abuu Daawuud na Ahmad kwa isnadi Swahiyh.
[4] al-Bukhaariy na Abuu Daawuud.
[5] al-Bukhaariy, Muslim na as-Siraaj.
[6] at-Tirmidhiy na al-Haakim aliyesema kuwa ni Swahiyh. Swahiyh at-Targhiyb (353).
[7] al-Bukhaariy na Abuu Daawuud.
[8] Abuu Daawuud na wengineo. Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan. Swahiyh at-Targhiyb (555).
[9] Ahmad na Abuu Ya´laa. (Swahiyh at-Targhiyb (556).
[10] al-Mukhallasw i ”Ahaadiyth Muntaqaat, at-Twabaraaniy, ar-Rawayaaniy, adh-Dhwiyaa’, Ibn Maajah, Ahmad na Ibn ´Asaakir. Swahiyh kwa mujibu wa Faqiyh al-Haythamiy katika “Asnaa al-Matwaalib””.
[11] Nguo ya pamba iliyofumwa.
[12] Nguo pana ambayo haikufumwa.
[13] al-Bukhaariy, Muslim na Maalik. Imetajwa katika ”al-Irwaa’”’” (376).
[14] Kijumba kidogo kilichofukiwa kidogo ardhini na kimeshabihiana na chumba cha kulalia au chumba cha kuhifadhia vitu. (an-Nihaayah)
[15] al-Bukhaariy, Muslim na Abuu ´Awaanah. Sababu – na Allaah ndiye mwenye kujua zaidi – ya ni kwa nini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuamrisha mapicha yachanwe na badala yake akatosheka na kuyaondo, ni kwa sababu hayakuwa na roho. Dalili ya hilo ni kwamba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyachana mapicha mengine, kama ilivyotajwa katika mapokezi katika al-Bukhaariy na Muslim. Anayetaka kutafiti haya zaidi arejee katika “Fath-ul-Baariy” (10/321) na ”Ghaayat-ul-Maraam fiy Takhriyj Ahaadiyth al-Halaal wal-Haraam ”(131-145).
[16] al-Bukhaariy na Muslim ilihali hiyo Hadiyth nyingne inamwendea Ibn Abiy Shaybah (12/110/2). Imetajwa katika ”al-Irwaa’” (8).
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 78-80
Imechapishwa: 13/10/2016
https://firqatunnajia.com/16-macho-yanatakiwa-kuangalia-mahala-pa-kusujudia-na-unyenyekevu-katika-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)