Allaah (Ta´ala) amemdhamini ambaye atashikamana na Qur-aan kwamba kamwe hatopotea duniani na wala hatokula maangamivu Aakhirah. Amesema (Ta´ala):
فَمَنِ اتَّبَعَ هُدَايَ فَلَا يَضِلُّ وَلَا يَشْقَى
”Basi atakayefuata uongofu Wangu hatopotea na wala kutaabika.”[1]
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Allaah amemkinga yule mwenye kufuata Qur-aan kutopotea duniani wala kula maangamivu.”
Amesema tena:
“Hatopotea duniani na wala hatokula maangamivu huko Aakhirah.”
Kisha akasoma:
فَمَنِ اتَّبَعَ هُدَايَ فَلَا يَضِلُّ وَلَا يَشْقَى
”Basi atakayefuata uongofu Wangu hatopotea na wala kutaabika.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Ambaye atajifunza Kitabu cha Allaah kisha akafuata yaliyomo ndani, basi Allaah atamlinda kutokamana na upotofu duniani na atamlinda pia na siku ya Qiyaamah na Hesabu mbaya.”[2]
[1] 20:123
[2] AmeipoekaRaziynkaamailivyokatika ”Mishkaat-ul-Maswaabiyh” (1/67).
- Muhusika: Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas Aal ´Abdil-Kariym
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hujaj al-Qawiyyah ´alaa anna Wasaa-il-ad-Da´wah Tawqiyfiyyah, uk. 21
- Imechapishwa: 07/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)