4 – ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
”Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anaswali Fajr walikuwa waumini wa kike wakiswali pamoja naye, wakijifunika nguo zao. Kisha wanarejea majumbani mwao na hakuna anayewatambua kutokana na giza.”[1]
Dalili hapa ni kwamba hawakuwa wanaweza kufahamika kutokana na giza. Maana yake ni kuwa wangefahamika kama kusingelikuwa giza. Wangelijulikana kikawaida kutokana na nyuso zao zilizofunuliwa. Hapo kumethibiti kile ninachokisema. Ijtihaad hiyo imenukuliwa na ash-Shawkaaniy (02/15) kutoka kwa al-Baajiy. Kisha baadaye nikapata upokezi mwingine unaosema wazi:
”Baadhi yetu tusingelijua nyuso za wengine.”
[1] al-Bukhaariy (372), Muslim (645) na wengineo. Nimeitaja katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (449).
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Jilbaab-ul-Mar-ah al-Muslimah, uk. 65-66
- Imechapishwa: 06/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)