Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Dalili ya uombezi ni maneno Yake (Ta´ala):
وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ وَيَقُولُونَ هَـٰؤُلَاءِ شُفَعَاؤُنَا عِندَ اللَّـهِ
“Na wanaabudu asiyekuwa Allaah ambao [hawawezi] kuwadhuru na wala kuwanufaisha na wanasema: “Hawa ni waombezi wetu mbele ya Allaah.”[1]
MAELEZO
Dalili ya madai yao ya kuomba uombezi ni maneno Yake (Ta´ala):
وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ وَيَقُولُونَ هَـٰؤُلَاءِ شُفَعَاؤُنَا عِندَ اللَّـهِ
“Na wanaabudu asiyekuwa Allaah ambao [hawawezi] kuwadhuru na wala kuwanufaisha na wanasema: “Hawa ni waombezi wetu mbele ya Allaah.”
Allaah akawaraddi kwa kusema:
قُلْ أَتُنَبِّئُونَ اللَّـهَ بِمَا لَا يَعْلَمُ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ
“Je, mnamjulisha Allaah kwa yale asiyoyajua katika mbingu na ardhini?”[2]
Je, nyinyi mnamjuza Allaah juu ya kitu asichokijua mbinguni na ardhini? Yeye (Subhaanah) hatambui kuwa Anaye mshirika katika ´ibaadah. Wao wanathibitisha uombezi na ukaribu. Hata hivyo Allaah akawakufurisha na kuwakadhibisha kwa kitendo hicho.
[1] 10:18
[2] 10:18
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Qawaa´id al-Arba´ah, uk. 137
- Imechapishwa: 05/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)