Miongoni mwazo ni maneno Yake (´Azza wa Jall):
قُلْ هَـٰذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّـهِ ۚ عَلَىٰ بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي
“Sema: “Hii ndio njia yangu: nalingania kwa Allaah, juu ya ujuzi na umaizi – mimi na anayenifuata.”[1]
Akabainisha (Subhaanah) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhiwa sallam) analingania kwa utambuzi na kwamba vivyo hivo ndio hali ya wafuasi wake. Hapa kuna fadhilah za ulinganizi na kwamba wafuasi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhiwa sallam) ndio wanaolingania katika njia yake kwa utambuzi. Utambuzi (البصير) ni ile elimu ya yale anayoyalingania na anayoyakataza. Hapa kuna utukufu na ubora wao.
[1] 12:108
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ad-Da´wah ilaa Allaah wa Akhlaaq-id-Du´aah, uk. 23
- Imechapishwa: 04/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)