4 – Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Jitofautisheni na washirikina! Punguzeni masharubu na zifugeni ndevu.”[1]
[1] al-Bukhaariy, Muslim, Abu ´Awaanah na al-Bayhaqiy kupitia kwa Naafiy´. Hata hivyo imekuja kwa Abu ´Awaanah:
”Jitofautisheni na waabudia moto.”
Hadiyth inatiliwa nguvu na nyingine aliyoipokea al-Bayhaqiy kupitia kwa Maymuun bin Mihraan, kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Umar ambaye amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitajiwa waabudia moto ambapo akasema: ”Hakika wao wanafuga masharubu yao na wananyoa ndevu zao. Jitofautisheni nao.”
Wasimulizi wake ni wenye kuaminika isipokuwa Abu Bakr Muhammad bin Ja´far al-Muzakkiy ambaye sijampata wasifu wake. Hata hivyo Ibn Hibbaan ameipokea kupitia njia nyingine na kwa ajili hiyo nimeitaja katika ”Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah” (2834). Vilevile inatiliwa nguvu na Hadiyth ya Abu Hurayrah inayokuja:
”Punguzeni masharubu na ziacheni ndevu na jitofautisheni na waabudia moto.”
Haafidhw Ibn Hajar amesema:
”Hiyo ndio maana ya Hadiyth ya Ibn ´Umar. Walikuwa wakipunguza ndevu zao na wengine katika wao walikuwa wakizinyoa.” (Fath-ul-Baariy)
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Jilbaab-ul-Mar-ah al-Muslimah, uk. 184
- Imechapishwa: 14/11/2023
4 – Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Jitofautisheni na washirikina! Punguzeni masharubu na zifugeni ndevu.”[1]
[1] al-Bukhaariy, Muslim, Abu ´Awaanah na al-Bayhaqiy kupitia kwa Naafiy´. Hata hivyo imekuja kwa Abu ´Awaanah:
”Jitofautisheni na waabudia moto.”
Hadiyth inatiliwa nguvu na nyingine aliyoipokea al-Bayhaqiy kupitia kwa Maymuun bin Mihraan, kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Umar ambaye amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitajiwa waabudia moto ambapo akasema: ”Hakika wao wanafuga masharubu yao na wananyoa ndevu zao. Jitofautisheni nao.”
Wasimulizi wake ni wenye kuaminika isipokuwa Abu Bakr Muhammad bin Ja´far al-Muzakkiy ambaye sijampata wasifu wake. Hata hivyo Ibn Hibbaan ameipokea kupitia njia nyingine na kwa ajili hiyo nimeitaja katika ”Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah” (2834). Vilevile inatiliwa nguvu na Hadiyth ya Abu Hurayrah inayokuja:
”Punguzeni masharubu na ziacheni ndevu na jitofautisheni na waabudia moto.”
Haafidhw Ibn Hajar amesema:
”Hiyo ndio maana ya Hadiyth ya Ibn ´Umar. Walikuwa wakipunguza ndevu zao na wengine katika wao walikuwa wakizinyoa.” (Fath-ul-Baariy)
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Jilbaab-ul-Mar-ah al-Muslimah, uk. 184
Imechapishwa: 14/11/2023
https://firqatunnajia.com/129-waislamu-wanapunguza-masharubu-na-wanafuga-ndevu-zao/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)