Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) amesema:
Katika Sunnah ni kuwakata Ahl-ul-Bid´ah na kujitenga nao mbali, kuacha mijadala na ugomvi katika dini na kutosoma vitabu vya wazushi na kutosikiliza maneno yao. Kila jambo jipya katika dini ni Bid´ah.
MAELEZO
Makusudio ya kuwakata Ahl-ul-Bid´ah ni kujitenga nao mbali, kuacha kuwapenda, kuacha kuwafanya ni marafiki, kuwasalimia, kuwatembelea na mfano wa hayo.
Kuwakata Ahl-ul-Bid´ah ni lazima. Amesema (Ta´ala):
لَّا تَجِدُ قَوْمًا يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ يُوَادُّونَ مَنْ حَادَّ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ
“Hutopata watu wanaomuamini Allaah na Siku ya Mwisho kuwa wanawapenda wale wanaopinzana na Allaah na Mtume Wake.”[1]
Isitoshe Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimkata Ka´b bin Maalik na rafiki yake wakati walipoacha kwenda katika vita vya Tabuuk[2].
Lakini hapana vibaya kufanya hivo ikiwa katika kukaa nao kuna manufaa, kuwabainishia haki na kuwatahadharisha kutokamana na Bid´ah. Pengine kufanya hivo ikawa ni jambo linalotatikana. Amesema (Ta´ala):
ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ وَجَادِلْهُم بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ
“Lingania katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha mazuri na jadiliana nao kwa ambayo ni mazuri zaidi.”[3]
Jambo hilo linaweza kuwa kwa kukaa nao na kuzungumza nao kama ambavyo kunaweza vilevile kukawa kwa kuwaandikia.
[1] 58:22
[2] al-Bukhaariy (4418) na Muslim (2769, 53). Rejea maneno kuhusu fiqh ya kisa hicho na zile faida na hukumu zinazopatikana ndani yake katika kitabu ”Zaad-ul-Ma´aad” (03/558) ya Ibn-ul-Qayyim.
[3] 16:125
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 158-159
- Imechapishwa: 19/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)