C- Kunywa maji ya usaha ya watu wa Motoni. Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah ameahidi kwamba yule mwenye kunywa pombe basi atamnyweshwa kutoka katika asili ya wazimu.” Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Ni nini hiyo asili ya wazimu?” Akasema: “Ni jasho la watu wa Motoni”, au “Usiri wa watu wa Motoni.”[1]
Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mola wangu ameapa kwa ufalme Wake: Mja wangu hatokunywa glasi ya pombe isipokuwa Nitamnywesha badala yake maji yenye moto ya Motoni, ni mamoja aliadhibiwa au alisamehewa.”[2]
Abu Muusa (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kufa ilihali ni mnywaji pombe, basi Allaah atamnywesha kutoka kwenye mto wa Ghutwah.” Kukasemwa: “Ni nini mto wa Ghutwah?” Akasema: “Ni mto unaopita kutoka kwenye nyuchi za makahaba.” Harufu mbaya inayotoka kwenye nyuchi zao itawaudhi watu wa Motoni.”[3]
Hapo kale alikuweko mlevi mmoja ambaye alipita karibu na kijiji kilichokuwa na kiwango kikubwa cha pombe ambapo akasoma mashairi yafuatayo:
Tiyzanaabaad zipo zabibu
kila ninapopita karibu hushangazwa
na wale wanaokunywa maji
Tahamaki akasikia sauti inayotoka chini ya mti ikisema:
Na Motoni yapo maji;
mtenda maasi hatokunywa glasi hata moja
isipokuwa matumbo yake yatayeyuka
[1] Muslim (2002).
[2] Ahmad (5/257).
[3] Ahmad (4/399) na Ibn Hibbaan (5346).
- Mhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Dhamm-ul-Khamr, uk. 16-18
- Imechapishwa: 22/07/2020
C- Kunywa maji ya usaha ya watu wa Motoni. Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah ameahidi kwamba yule mwenye kunywa pombe basi atamnyweshwa kutoka katika asili ya wazimu.” Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Ni nini hiyo asili ya wazimu?” Akasema: “Ni jasho la watu wa Motoni”, au “Usiri wa watu wa Motoni.”[1]
Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mola wangu ameapa kwa ufalme Wake: Mja wangu hatokunywa glasi ya pombe isipokuwa Nitamnywesha badala yake maji yenye moto ya Motoni, ni mamoja aliadhibiwa au alisamehewa.”[2]
Abu Muusa (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kufa ilihali ni mnywaji pombe, basi Allaah atamnywesha kutoka kwenye mto wa Ghutwah.” Kukasemwa: “Ni nini mto wa Ghutwah?” Akasema: “Ni mto unaopita kutoka kwenye nyuchi za makahaba.” Harufu mbaya inayotoka kwenye nyuchi zao itawaudhi watu wa Motoni.”[3]
Hapo kale alikuweko mlevi mmoja ambaye alipita karibu na kijiji kilichokuwa na kiwango kikubwa cha pombe ambapo akasoma mashairi yafuatayo:
Tiyzanaabaad zipo zabibu
kila ninapopita karibu hushangazwa
na wale wanaokunywa maji
Tahamaki akasikia sauti inayotoka chini ya mti ikisema:
Na Motoni yapo maji;
mtenda maasi hatokunywa glasi hata moja
isipokuwa matumbo yake yatayeyuka
[1] Muslim (2002).
[2] Ahmad (5/257).
[3] Ahmad (4/399) na Ibn Hibbaan (5346).
Mhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Dhamm-ul-Khamr, uk. 16-18
Imechapishwa: 22/07/2020
https://firqatunnajia.com/07-kinywaji-cha-mnywaji-pombe-motoni/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)