163 – Abu Hurayrah amesema:
“Siku moja tulikuwa tukitembea pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) tukayapitia makaburi mawili. Akasimama na sisi tukasimama. Rangi ya uso wake ikabadilika mpaka ikajikunja mikono ya kanzu yake. Tukasema: “Ni nini, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: “Kwani hamsikii kile ninachosikia?” Tukasema: “Ni kipi, ee Nabii wa Allaah?” Akasema: “Mabwana hawa wawili wanaadhibiwa ndani ya makaburi yao adhabu kali kwa kitu chepesi.” Tukauliza sababu ambapo akasema: “Mmoja wao alikuwa hajikingi na mkojo na huyo mwingine alikuwa akiwaudhi watu kwa ulimi wake na akieneza umbea kati yao.” Akaitisha makuti mawili ya mtende na akaweka moja katika kila kaburi.” Tukasema: “Je, hayawafaa?” Akasema: “Ndio. Itafanywa nyepesi adhabu yao muda wa kuwa bado ni kijani.”[1]
Ameipokea Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh” yake.
Maneno yake kwamba dhambi ilikuwa nyepesi maana yake ni kwamba walikuwa wakidhani kuwa ni nyepesi au kwamba ilikuwa vyepesi kuiepuka, na si kuwa ukweli wa mambo yenyewe kama yenyewe ilikuwa nyepesi. Kwa sababu uvumi ni kitu kilichoharamishwa kwa maafikiano.
[1] Swahiyh.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/178-179)
- Imechapishwa: 05/04/2021
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
163 – Abu Hurayrah amesema:
“Siku moja tulikuwa tukitembea pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) tukayapitia makaburi mawili. Akasimama na sisi tukasimama. Rangi ya uso wake ikabadilika mpaka ikajikunja mikono ya kanzu yake. Tukasema: “Ni nini, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: “Kwani hamsikii kile ninachosikia?” Tukasema: “Ni kipi, ee Nabii wa Allaah?” Akasema: “Mabwana hawa wawili wanaadhibiwa ndani ya makaburi yao adhabu kali kwa kitu chepesi.” Tukauliza sababu ambapo akasema: “Mmoja wao alikuwa hajikingi na mkojo na huyo mwingine alikuwa akiwaudhi watu kwa ulimi wake na akieneza umbea kati yao.” Akaitisha makuti mawili ya mtende na akaweka moja katika kila kaburi.” Tukasema: “Je, hayawafaa?” Akasema: “Ndio. Itafanywa nyepesi adhabu yao muda wa kuwa bado ni kijani.”[1]
Ameipokea Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh” yake.
Maneno yake kwamba dhambi ilikuwa nyepesi maana yake ni kwamba walikuwa wakidhani kuwa ni nyepesi au kwamba ilikuwa vyepesi kuiepuka, na si kuwa ukweli wa mambo yenyewe kama yenyewe ilikuwa nyepesi. Kwa sababu uvumi ni kitu kilichoharamishwa kwa maafikiano.
[1] Swahiyh.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/178-179)
Imechapishwa: 05/04/2021
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/07-hadiyth-mabwana-hawa-wawili-wanaadhibiwa-ndani-ya-makaburi-yao-adhabu-kali/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)